Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Makala

UN Photo/Tobin Jones

WFP kuongeza usaidizi katika pembe ya Afrika

Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani WFP limetangaza kuongeza usaidizi katika Pembe ya Afrika wakati huu ambapo kiwango cha njaa kinazidi kuongezeka baada ya ukame wa mfululizo, na tishio la njaa linazidi kutanda.

Tangu kuanza kwa mwaka huu, zaidi ya watu milioni tisa wameingia katika uhaba mkubwa wa chakula kote katika nchi za Ethiopia, Kenya, na Somalia, na kuwaacha watu milioni 22 wakihangaika kupata chakula cha kutosha.

Sauti
4'30"
UN News/Assumpta Massoi

Asante UNDP Tanzania sasa wanawake Kigoma tunaona matunda ya kuweko kwenye vikundi

Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa maendeleo duniani, UNDP limejizatiti kusaidia mipango ya kuinua wanawake na vijana kwa  kupatia makundi hayo mitaji. Hilo linafanyika mkoani Kigoma nchini Tanzania ambako uweko wa wakimbizi ulibainika kuleta changamoto katika upatikanaji wa  mahitaji siyo tu kwa wakimbizi bali pia kwa jamii za wenyeji ambao wanawapatia hifadhi.

Sauti
4'46"
FAO

Chukua hatua zifuatazo kuepusha sumu kuvu kwenye mazao

Umoja wa Mataifa kupitia mashirika yake ikiwemo lile la chakula na kilimo, FAO pamoja na lile la afya duniani, WHO yanapigia chepuo umuhimu wa kukabiliana na sumu kuvu kwenye mazao. Hii ni kwa kutambua kuwa sumu kuvu sio tu ina madhara kwa afya ya binadamu bali pia ni moja ya sababu kubwa ya upotevu wa mavuno ya mazao. Uhifadhi duni wa mazao kama vile mahindi, karanga husababisha mazao hayo kupata sumu kuvu na hivyo yasiweze kuuzika na pia iwapo mtu atanunua na kula basi anaweza kupata madhara ya kiafya. Je sumu kuvu ni nini?

Sauti
3'26"
UN/Anold Kayanda

TEDI Tanzania tunalenga kuhamasisha kuwe elimu inayoendana na hali ya sasa duniani

Asasi isiyo ya kiserikali ya TEDI Tanzania, katika kutekeleza Lengo namba 4 la Maendeleo Endelevu linalohusu elimu bora, imeamua kulitekeleza lengo hilo kupitia kampeni yao ya kuishawishi serikali na wadau wengine kuboresha ubora wa elimu nchini Tanzania kuanzia ngazi ya msingi hadi taasisi ya elimu ya juu kwa kuziba pengo kati ya nadharia na vitendo kupitia kuunganisha ujuzi wa vitendo ambao hautolewi katika mtaala wa kawaida wa elimu elimu. Gloria Anderson, Mkurugenzi wa shirika la TEDI Tanzania ambalo linahamasisha elimu inayoendana na hali ya sasa ya sayansi na teknolojia ili

Sauti
4'8"
MONUSCO/TANZBATT_9

Kiswahili: Juhudi binafsi za kukiendeleza sambamba na kinavyoleta ahueni kwa walioko kwenye mizozo

Zaidi ya mwezi sasa umepita tangu maadhimisho ya kwanza ya lugha ya Kiswahili duniani na harakati zinaendelea kusongesha lugha hiyo adhimu. Ni katika nyakati kama hizo watu wanaanza kutambua umuhimu wa lugha yoyote katika maendeleo na hadi kupatiwa hadhi ya kimataifa inakuwa juhudi nyingi zimefanyika. Ziko juhudi binafsi, za kikanda na za kimataifa ambazo zinawezesha lugha kutumika hata pale penye mazingira magumu ili kuleta ahueni kwa wenyeji.
Sauti
4'8"
Leah Mushi

Vijana tuaminiwe tunapoanzisha mashirika - Suzan

Tarehe 12 mwezi huu wa Agosti dunia itaadhimisha siku ya Vijana duniani chini ya kauli mbiu Mshikamano wa vizazi: Kuunda Ulimwengu kwa Vizazi vyote, lengo likiwa kuhakikisha rika zote kwenye jamii zina mshikamano na vijana wanaweza kufikia malengo ikiwa ni pamoja na kutafuta suluhu za changamoto katika jamii zinazowazunguka.

Sauti
4'1"
MINUSCA/TANZBAT-5

TANZBATT 5 wachangia damu katika hospitali ya Berberati, CAR

Wanajeshi walinda amani wa TANZBATT 5 ambacho ni kikosi cha 5 kutoka Tanzania wanaohudumu katika Ujumbe wa Umoja wa Mataifa unaolinda amani nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, MINUSCA, mara kwa mara wanaweka bunduki chini na kushiriki shughuli mbalimbali za kijamii kama vile usafi wa mazingira na michezo. Safari hii wameshiriki katika utchangiaji wa damu ili kuunga mkono juhudi za serikali ya CAR kuwatibu watoto waliozaliwa na midomo iliyochanika, yaani midomo sungura. Afisa Habari wa TANZBATT 5 Meja Asia Hussein, anaripoti.

Sauti
2'55"
© UNOCHA/Endurance Lum Nji

Hali mwanzoni ilikuwa mbaya sasa UNHCR imetusaidia- Mkimbizi DRC

Hali si shwari kwa makumi ya maelfu ya wakimbizi na wakimbizi wa ndani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC kutokana na kuendelea kufurushwa makwao kutokana na ghasia zinazochochewa na vikundi vilivyojihami mashariki mwa nchi hiyo. Mahitaji ya kibinadamu yanaongezeka kila uchao huku ufadhili kwa mashirika kama lile la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR ukipungua.

Lakini shirika hilo linajitahidi kuwapatia wakimbizi msaada wa kimkakati ili waweze kujitegemea. Wako walionufaika na wengine wanahitaji usaidizi zaidi kwa watoot wao waweze kwenda shuleni.

Sauti
3'58"