WFP kuongeza usaidizi katika pembe ya Afrika
Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani WFP limetangaza kuongeza usaidizi katika Pembe ya Afrika wakati huu ambapo kiwango cha njaa kinazidi kuongezeka baada ya ukame wa mfululizo, na tishio la njaa linazidi kutanda.
Tangu kuanza kwa mwaka huu, zaidi ya watu milioni tisa wameingia katika uhaba mkubwa wa chakula kote katika nchi za Ethiopia, Kenya, na Somalia, na kuwaacha watu milioni 22 wakihangaika kupata chakula cha kutosha.