Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Makala

© WFP/Sandaeric Nirinarison

Umoja wa Mataifa waendelea kutoa misaada ya dharura Madagascar

Kwa kipindi cha mwezi mmoja tu, nchi ya Madagascar imekabiliana na vimbunga vinne. Jumanne iliyopita, kimbunga Emnati kiliathiri maeno yaleyale yaliyoathirika na kimbunga Batsirai na kuwafurusha makwao maelfu ya watu. Umoja wa Mataifa unashirikiana na wadau wa kibinadamu na serikali ya Madagascar kuwasaidia wale wanaohitaji misaada ya dharura.

Sauti
2'13"
UNFPA/ Warren Bright

Ushiriki wa viongozi wa dini katika kupambana na ukeketaji Tarime Tanzania waanza kuonesha mwanga

Ukeketaji unajumuisha taratibu zote zinazohusisha uondoaji wa sehemu au jumla yote ya sehemu ya siri ya nje ya mwanamke. Zoezi hilo mara nyingi hufanywa na waganga wa jadi na wanaokeketa wanajulikana kama mangariba.  Ukeketaji unatambulika kimataifa kama ukiukaji wa haki za binadamu za wasichana na wanawake.

Umoja wa Mataifa umekuwa ukichagiza mbinu mbalimbali za kutokomeza vitendo hivi vya kikatili na nchi wanachama zimepokea wito huo na kutafuta namba tofautofauti za kupambana na hali hiyo ambayo imejikita katika utamaduni wa baadhi ya jamii ulimwenguni.

Audio Duration
3'15"
UN News

Sawa Wanawake Tanzania yakabidhi majengo mawili kwa serikali ya Tanzania kusaidia vita dhidi ya unyanyasaji wa watoto

Mwishoni mwa mwaka jana 2021, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF lilisema mwaka huo ulikuwa wa machungu na ukiukwaji mkubwa wa haki za watoto. Ingawa taarifa ya UNICEF ililenga katika mizozo ya muda mrefu na ile mipya ni wazi kuwa matukio ya ukiukwaji wa haki za watoto na unyanyasaji dhidi yao, unaendelea kujidhihirisha katika maeneo mbalimbali duniani.

Sauti
4'2"
FAO Tanzania

Salvation Youth Group wa Kasulu Kigoma Tanzania waushukuru mradi wa KJP 

Mnamo mwaka 2017 mashirika ya Umoja wa Mataifa lile la Chakula na Kilimo FAO, la Mpango wa Chakula Duniani WFP kwa kushirikiana na Shirika la kimataifa la maendeleo ya mitaji UNCDF pia Kituo cha Biashara cha kimataifa ITC, yaliamua kushirikiana kutekeleza mradi wa pamoja Mkoani Kigoma nchini Tanzania, KJP. Kupitia mradi huo unaowahusisha wanawake vijana na wanaume vijana kupitia kwenye vikundi vyao, kikundi cha Salvation Youth Group cha Kasulu Kigoma kimenufaika kwa kupewa mashine ya kutotolesha vifaranga vya kuku kupitia mradi huo.

Sauti
3'21"
UN SDGs

Vijana wanaweza kuchagiza SDGs ikiwa watapewa miongozo sahihi - Austine Oduor

Vijana wanaaminika kuwa kundi muhimu katika kufanikisha malengo ya maendeleo endelevu, SDGs kwani nguvu yao ikikutana na ubunifu, inaweza kufanikisha mambo mengi chanya kwa ulimwengu. Hata hivyo kundi hili likikosa miongozo na taarifa sahihi linaweza kuwa kikwazo cha maendeleo yanayotarajiwa. Ndio maana Austine Oduor wa nchini Kenya, aliamua kuanzisha miradi inayowasaidia vijana wa mtaa wa mabanda wa Mukuru kwa Njenga jijini Nairobi, Kenya ili waweze kuanzisha biashara zao na pia kuwapa ushauri kuhusu maisha bora kuwaepusha na uhalifu.

Sauti
3'17"
Patrick Zachmann/Magnum Photos for FAO

Tutumie elimu tulizonazo kwa vitendo kwa ajili ya ustawi wa jamii zetu – Dkt. Anthony Kiiza 

Ufugaji na kilimo ni moja ya mambo mtambuka ambayo yakifanikiwa yanachangia katika kufanikisha idadi kubwa ya malengo ya Umoja wa Mataifa ya maendeleo endelevu, SDGs kati ya 17 ambayo yanalengwa kufikiwa ifikapo mwishoni mwa muongo huu, mwaka 2030.  

Mathalani lengo namba moja linazungumzia kutokomeza umaskini, namba mbili linaongelea kutokomeza njaa, namba tatu linaongelea afya bora, namba saba linazungumzia nishati bora na ambayo ni nafuu na lengo namba nane likizungumzia ukuaji wa uchumi. Malengo yote hayo yanaguswa moja kwa moja na kilimo.  

Sauti
3'48"
UN SDGs

Mkopo wa masharti nafuu kwa vijana Tanzania waleta kipato na kufungua ajira

Umoja wa Mataifa kupitia malengo yake ya maendeleo endelevu, SDGs ya mwaka 2015 unataka vijana wapatiwe kipaumbele katika kufanikisha malengo hayo ikiwemo namba moja la kutokomeza umaskini. Serikali zinachagizwa kuweka mazingira wezeshi kwa vijana kujiajiri na ndio maana nchini Tanzania mikopo isiyo na masharti kwa vijana imekuwa mkombozi kwa vijana mkoani Mbeya ambapo takribani vijana 10 mjini Tukuyu wilaya ya Rungwe wametumia mkopo waliopatiwa kununua mashine ya kisasa ya kufyatua matofali.

Sauti
3'24"