Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Makala

UN News/ John Kibego

Mchakato wa kuomba makazi katika nchi ya tatu ukirejea tutafurahi sana - Wakimbizi Kyangwali Uganda 

Mlipuko wa COVID-19 ulififiza mambo mengi ikiwemo mchakato wa wakimbizi kuomba hifadhi katika nchi ya tatu ambapo huwa na matarajio makubwa kama maisha kuwa bora na upatikanaji wa kazi. Wakimbizi huwa na matarajio mengi kuhusu kupatiwa hifadhi katika nchi ya pili ya ukimbizi kutokana na simulizi wanazosikia kutoka wenzao waliowatangulia kwenda ng’ambo. Hata hivyo ndoto zao ziikuwa zimetiwa mashakani na mlipuko wa COVID-19 ambapo mchakato wa kuomba hifadhi ulisitishwa.

Sauti
3'48"
UNDP Bangladesh/Fahad Kaizer

Nilishuhudia shida wanazopitia wenye ulemavu nikatafuta ufumbuzi

Umoja wa Mataifa unaamini uvumbuzi na ubunifu ni moja ya nyenzo za kufanikisha kuyatimiza malengo ya maendeleo endelevu, SDGs. Kwa wale ambao wamelielewa somo hilo, tayari wanafanyia kazi ushauri huo na kuleta mabadiliko chanya katika jamii zao. Mfano ni fundi Lincoln Wamae wa nchini Kenya.


Lincold Kenya anasema kutokana na alivyokuwa anaziona changamoto zinazowakabili watu wenye ulemavu nchini mwake wanapokuwa wanaenda na kurejea kutoka katika shughuli zao za kila siku, kulimfanya kuanza kuwaza namna ya kubuni viti mwendo vya kuwasaidia.

Sauti
3'10"
Manglar Vivo Project, UNDP Cuba

Mikopo kwa Miradi ya Mazingira kuwa na riba rafiki : CRDB Bank Tanzania

Katika makala hii leo Stella Vuzo wa Kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa, UNIC Dar es salaam nchini Tanzania amezungumza na Hailo Kabiki mtaalamu wa masuala ya mazingira wa benki ya CRDB nchini Tanzania ambayo mwezi Oktoba mwaka jana wa 2021ilipata dola milioni 100 kutoka mfuko wa mazingira duniani, GCF kufanikisha kilimo kinachojali mazingira.

Na Benki yenyewe ikatenga dola milioni 100 na hivyo kufanya iwe na dola milioni 200 za kukopesha watakaokidhi vigezo. Katika mahojiano haya Bwana Kabiki anaanza kwa kuelezea mradi huo na mchakato wake.

Sauti
3'43"