Mchakato wa kuomba makazi katika nchi ya tatu ukirejea tutafurahi sana - Wakimbizi Kyangwali Uganda
Mlipuko wa COVID-19 ulififiza mambo mengi ikiwemo mchakato wa wakimbizi kuomba hifadhi katika nchi ya tatu ambapo huwa na matarajio makubwa kama maisha kuwa bora na upatikanaji wa kazi. Wakimbizi huwa na matarajio mengi kuhusu kupatiwa hifadhi katika nchi ya pili ya ukimbizi kutokana na simulizi wanazosikia kutoka wenzao waliowatangulia kwenda ng’ambo. Hata hivyo ndoto zao ziikuwa zimetiwa mashakani na mlipuko wa COVID-19 ambapo mchakato wa kuomba hifadhi ulisitishwa.