Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

WFP kuongeza usaidizi katika pembe ya Afrika

WFP kuongeza usaidizi katika pembe ya Afrika

Pakua

Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani WFP limetangaza kuongeza usaidizi katika Pembe ya Afrika wakati huu ambapo kiwango cha njaa kinazidi kuongezeka baada ya ukame wa mfululizo, na tishio la njaa linazidi kutanda.

Tangu kuanza kwa mwaka huu, zaidi ya watu milioni tisa wameingia katika uhaba mkubwa wa chakula kote katika nchi za Ethiopia, Kenya, na Somalia, na kuwaacha watu milioni 22 wakihangaika kupata chakula cha kutosha.

Mkurugenzi Mtendaji wa WFP David Beasley siku wiki iliyopita akufanya ziara katika nchi za Pembe ya Afrika ikiwemo Somalia nchi iliyokumbwa na ukame, ambako zaidi ya watu milioni saba ambao ni takriban nusu ya wakazi wake wana uhaba wa chakula na watu 213,000 tayari wanakabiliwa na hali kama ya njaa.

Tuungane na Evarist Mapesa anayetuletea yote aliyokutana nayo Mkuu huyo wa WFP.
 

Audio Credit
Leah Mushi /Evarist Mapesa
Sauti
4'30"
Photo Credit
UN Photo/Tobin Jones