Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Jarida la Habari

© UNICEF/Ahmed Amin Ahmed Mohamed Osman

UNFPA inasaidia kuhakikisha uzazi salama kwa wanawake na wasichana wanaokimbia ghasia Khartoum

Wanawake na wasichana wanaokimbia machafuko yanayoendelea mjini Kharthoum nchini Sudan wanakabiliwa na changamoto lukuki hususan kwa wajawazito wanaohitaji msaada wa kujifungua, kwa mujibu wa shirika la Umoja wa Mataifa la idadi ya watu na afya ya uzazi UNFPA ambalo sasa limechukua jukumu la kuhakikisha uzazi salama kwa wanawake hao. 

Sauti
2'51"

30 JUNI 2023

Hii leo jaridani tunaangazia wanawake na wasichana nchini Sudan na kazi ya walinda amani nchini CAR. Makala tutakupeleka nchini DRC na mashinani nchini Misri, kulikoni?

Sauti
13'4"

29 JUNI 2023

Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ambapo tukiwa tunaelekea maadhimisho ya pili ya siku ya kimataifa ya lugha ya Kiswahili duniani leo tunaelekea nchini Uganda kuangazia hatua zinazopigwa kufuta kabisa usemi wa mitaani kuwa Kiswahili kilizaliwa Tanzania, kikafa Kenya na kisha kuzikwa Uganda. Pia tunakuletea habari kwa ufupi zikiwemo za WHO, UNICEF na FAO. Katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo nampisha Dkt. Mwanahija Ally Juma akitujuza walivyojiandaa kuadhimisha siku ya lugha ya Kiswahili duniani ambayo kilele chake ni Julai 7.

Sauti
15'37"

27 JUNI 2023

Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ambayo leo inaturejesha hapa Makao makuu ya umoja wa Mataifa kusiki maandalizi ya maadhimisho ya pili ya siku ya Lugha ya Kiswahili duniani. Pia tunakuletea habari kwa ufupi zikiwemo ripoti ya Katibu Mkuu kuhusu watoto katika migogoro ya silaha, msaada kwa wakimbizi nchini Sudan na maadili ya akili bandia. Katika mashinani tunakupeleka nchini Mali, kulikoni?

Sauti
15'49"

26 JUNI 2023

Hii leo jaridani tunaangazia lugha ya Kiswhaili na ripoti ya dawa za Kulevya ya UNODC 2023. Makala tunakupeleka nchini Pakistan na mashinani nchini Kenya, kulikoni?

Sauti
13'26"
TANBAT 6/Kapteni Inyoma

CAR: Walinda amani wa UN kutoka Tanzania na Senegal wafanya mazoezi ya pamoja

Walinda amani wa Umoja wa Mataifa wa kikosi cha 6 kutoka Tanzania (TANBAT 6) na wenzao kutoka kikosi cha polisi kinachotoka Senegal wote wakihudumu chini ya Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamuhuri wa Afrika ya Kati (MINUSCA), kwa wiki nzima wamefanya mazoezi ya pamoja ya ulinzi wa amani na kutuliza ghasia hususani wakati nchi hiyo ikijiandaa na uchaguzi wa ngazi mbalimbali ikiwemo kura ya maoni kuhusu katiba.

Sauti
2'51"

23 JUNI 2023

Hii leo jaridani tunaangazia umuhimu wa watumishi wa umma na walinda amani nchini Jamhuri ya Afrika ya kati. Makala tunakupeleka nchini Kenya na mashinani nchini Afrika Kusinin, kulikoni?

Sauti
10'41"

22 JUNI 2023

Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ambayo inatupeleka Kenya kuangazia awamu ya pili ya mradi wa PLEAD unaoendesha na ofisi ya Umoja wa Mataifa ya dawa na uhalifu UNODC nchini Kenya. Pia tunakuletea habari kwa ufupi zikiwemo za msaada kwa wakulima nchini Ukraine, ripoti ya UNICEF kuhusu watoto katika hatari kubwa ya athari za janga la tabianchi na hafla ya ufunguzi wa Mkutano wa Mkataba Mpya wa Ufadhili wa Kimataifa Paris.

Sauti
12'36"

21 JUNI 2023

Hii leo jaridani tunaangazia Migogoro nchini Ukraine na wakimbizi nchini Kenya. Makala tunakupeleka nchini Tanznai na mashinani tunasalia hapa hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa, kulikoni?  

Sauti
13'20"