15 Oktoba 2021
Ni Ijumaa ya tarehe 15 mwezi Oktoba mwaka 2021 siku ya kimataifa ya wanawake wa vijijini.
Karibu uungane na Flora Nducha kusikiliza jarida ambapo kama ilivyo ada ijumaa ni siku ya kuwa na mada kwa kina na hii leo tunamulika afya ya akili tukifunga safari hadi Kenya kwa msichana aliyetaka kujiua, kulikoni?
Pia utapata fursa ya kujifunza lugha ya Kiswahili ambapo leo tunapata ufafanuzi wa maana za neno "KITAMBI" na mchambuzi wetu ni Onni Sigalla Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania , BAKITA.