Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari kwa Ujumla

©FAO/Atul Loke

FAO: Kuna nishati safi na fedha katika kinachoonekana kuwa ni takataka

Kilimo ni moja ya shughuli za kibinadamu zinazochangia katika uchafuzi wa hewa. Kwa kulitambua hilo, FAO kote ulimwenguni inachagiza kile inachokiita kwa lugha ya kiingereza Bioeconomy yaani uchumi ambao msingi wake unatokana na matumizi ya rasilimali za kibayolojia zinazopatikana kwenye mazingira; kwa mfano kurejesha taka katika uzalishaji wa nishati safi, mbadala wa mafuta ya kisukuku.

Sauti
1'42"
© UNICEF/Milequem Diarassouba

Siku ya Elimu Duliani 2024 yatumika kukabiliana na kauli za chuki

Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) limeyatumia maadhimisho ya mwaka huu ya Siku ya Kimataifa ya Elimu kuangazia jukumu muhimu la elimu na walimu katika kukabiliana na kauli za chuki, jambo ambalo limekithiri katika miaka ya hivi karibuni kutokana na matumizi ya mitandao ya kijamii na hivyo kuharibu muundo wa jamii kote duniani. 

Sauti
2'10"
UN News

Uganda: Makazi ya wakimbizi yatumia elimu kusongesha amani miongoni mwa wakimbizi

Nchini Uganda katika makazi ya wakimbizi ya Kyangwali wilaya ya Kikuube magharibi mwa taifa hilo, suala la mchango wa elimu kwenye amani liko dhahiri kwani tulipotembelea katika makazi hayo, Yahya Kato ambaye ni Mwalimu Mkuu katika Shule ya msingi Kasonga kwenye makazi hayo ya wakimbizi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC na Sudan aliteueleza kile wanachofanya. 

Sauti
1'15"
© UNICEF/Eyad El Baba

UN: Raia 25, 000 wamepoteza maisha katika vita Gaza na mahitaji ya kibinadamu yanazidi kuongezeka

Mashambulizi makubwa ya mabomu yanayofanywa na Israel Gaza yameendelea tena leo sanjari na maroketi yanayovurumushwa na makundi yenye silaha ya Kipalestina kuelekea Israel, wakati wahudumu wa kibinadamu wa Umoja wa Mataifa wakiripoti kuuawa kwa watu zaidi ya 25,000 Gaza tangu kuanza kwa machafuko hayo mapya Oktoba 7 mwaka jana na mahitaji ya kibinadamu yakiongezeka kila uchao. 

Hali inazidi kubwa mbaya na hakuna dalili ya kukomesha uhasama Gaza limesema shirika la Umoja wa Mataifa la kuratibu misaada ya kibinadamu na masuala ya dharura OCHA. 

Sauti
2'22"
Photo: OCHA Burundi / Ana Maria Pereira

Nchini Burundi mbinu ya mashangazi na baba wa shuleni yaepusha watoto na kejeli kutoka kwa wenzao

Nchini Burundi shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF limechukua hatua kuhakikisha watoto wakimbizi wanaorejea nchini humo wanaweza kuendelea na elimu bila uoga na jakamoyo hasa pale wanapokumbana na vizuizi vya tofauti ya lugha waliyotumia ukimbizini na ile inayotumika nyumbani walikorejea. 

Hebu fikiria baada ya machungu ya ukimbizini, unarejea nyumbani nako shuleni unakumbwa na kejeli kisa tu matamshi ya lugha utumiayo ni tofauti na yale ya wenzako darasani. 

Sauti
2'21"
© FAO/Luis Tato

Kaveh Zahedi wa FAO: Hatuwezi kuwa tu watazamaji wa mabadiliko ya tabianchi, kilimo kina jukumu

Kilimo kinaweza kuchukua jukumu kuu katika hatua dhidi ya tabianchi wakati huo huo kikihakikisha uhakika wa chakula duniani, ni maoni ya Mkurugenzi wa Ofisi ya Mabadiliko ya Tabianchi, Bayonuai na Mazingira katika Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo (FAO) Kaveh Zahedi kufuatia hivi majuzi mwaka 2023 kuthibitishwa kuwa mwaka wa joto zaidi katika rekodi za dunia. 

Sauti
1'18"
© UNICEF/Eyad El Baba

UN yaomba kufunguliwe njia nyingine ya kufikisha misaada Gaza

Zikiwa ni zaidi ya siku 100 tangu kuibuka upya kwa mzozo huko Mashariki ya Kati, mashirika ya Umoja wa Mataifa hii leo wametoa taarifa inayoeleza kuongezeka kwa hatari ya baa la njaa na milipuko ya magonjwa ya kuambukiza huku yakisisitiza muarobaini pekee kwa sasa ni kuruhusu njia mpya za kuingiza misaada ya kwenda kutatua changamoto zinazowakabili wananchi walioko Gaza. 

Sauti
3'34"