Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari kwa Ujumla

UNHCR/L. Godinho

Kamishna Mkuu wa UNHCR akiwa ziarani Ethiopia anasihi wasisahaulike wanaoikimbia Sudan

Kamishna Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR), Filippo Grandi akihitimisha ziara ya siku tatu nchini Ethiopia ametoa wito kwa ulimwengu kuwasaidia watu wa Sudan wanaoikimbia nchi yao na kuingia Ethiopia ambayo ni moja ya nchi wenyeji wa wakimbizi na wakimbizi wa ndani wengi zaidi ulimwenguni. 

“Kuna majanga mengine kote duniani. Mengine makali zaidi na mengine yanaongelewa zaidi. Tusiwasahau watu ambao nimezungumza nao waliokimbia vita Sudan. Hawa wanateseka kila siku na wanahitaji msaada.”

Sauti
1'31"
UNHCR Video

Simulizi ya Islam Mubarak: Ndoto yangu ni kurejea nyumbani na kuishi kwa amani

Kutana na Islam Mubarak msichana mwenye umri wa miaka 21 ambaye vita mpya iliyozuka Sudan Aprili mwaka jana ilimlazimisha kufungasha virago na familia yake na kuukimbia mji mkuu Khartoum na sasa amekwama katika kambi ya wakimbizi wa ndani katika jimbo la El-Gedarif, lakini ndoto yake ni kurejea nyumbani siku moja.

Katika kambi ya wakimbizi wa ndani inayosimamiwa na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR ni Islam akiwa amekata tamaa kwa kutouona au kuelezea mustakbali wake .

Sauti
2'30"
©UNDP Syria – Zuhir-Al Fourati

Mashamba darasa yaliyoandaliwa na FAO Syria yainua wanawake wafugaji

Na sasa tuelekee Mashariki ya Kati, Leah Mushi anatueleza jinsi mashirika ya Umoja wa Mataifa lile la Chakula na Kilimo FAO na la Mpango wa chakula duniani WFP yanavyosaidia kuinua maisha ya wananchi katika nchi ya Syria.

Mashariki mwa Syria katika mji wa Deir ez-Zor ulioko umbali wa km 450 kutoka mji mkuu wa nchi hiyo Damascus, mashirika ya UN lile la FAO na WFP yanafanya kila juhudi kuwajengea uwezo na kubadili maisha ya wananchi kupitia miradi mbalimbali.

Sauti
1'42"
© ICJ-CIJ/ Frank van Beek

Mahakama ya Kimataifa ya Haki, ICJ yaitaka Israeli iepushe mauaji ya kimbari Gaza

Mahakama ya Kimataifa ya Haki, ICJ hii leo imeamua kuwa Israel lazima ichukue hatua zote za kuzuia vitendo vya mauaji ya kimbari katika mashambulizi yake dhidi ya wapalestina huko, Gaza, uamuzi unaofuatia shauri lililowasilishwa na Afrika Kusini la kutaka Mahakama hiyo ya Umoja wa Mataifa ichukue hatua za awali kwa mujibu wa Mkataba wa kimataifa wa kuepusha mauaji ya kimbari wa mwaka 1948. 

Sauti
2'13"
©FAO/Atul Loke

FAO: Kuna nishati safi na fedha katika kinachoonekana kuwa ni takataka

Kilimo ni moja ya shughuli za kibinadamu zinazochangia katika uchafuzi wa hewa. Kwa kulitambua hilo, FAO kote ulimwenguni inachagiza kile inachokiita kwa lugha ya kiingereza Bioeconomy yaani uchumi ambao msingi wake unatokana na matumizi ya rasilimali za kibayolojia zinazopatikana kwenye mazingira; kwa mfano kurejesha taka katika uzalishaji wa nishati safi, mbadala wa mafuta ya kisukuku.

Sauti
1'42"
© UNICEF/Milequem Diarassouba

Siku ya Elimu Duliani 2024 yatumika kukabiliana na kauli za chuki

Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) limeyatumia maadhimisho ya mwaka huu ya Siku ya Kimataifa ya Elimu kuangazia jukumu muhimu la elimu na walimu katika kukabiliana na kauli za chuki, jambo ambalo limekithiri katika miaka ya hivi karibuni kutokana na matumizi ya mitandao ya kijamii na hivyo kuharibu muundo wa jamii kote duniani. 

Sauti
2'10"
UN News

Uganda: Makazi ya wakimbizi yatumia elimu kusongesha amani miongoni mwa wakimbizi

Nchini Uganda katika makazi ya wakimbizi ya Kyangwali wilaya ya Kikuube magharibi mwa taifa hilo, suala la mchango wa elimu kwenye amani liko dhahiri kwani tulipotembelea katika makazi hayo, Yahya Kato ambaye ni Mwalimu Mkuu katika Shule ya msingi Kasonga kwenye makazi hayo ya wakimbizi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC na Sudan aliteueleza kile wanachofanya. 

Sauti
1'15"
© UNICEF/Eyad El Baba

UN: Raia 25, 000 wamepoteza maisha katika vita Gaza na mahitaji ya kibinadamu yanazidi kuongezeka

Mashambulizi makubwa ya mabomu yanayofanywa na Israel Gaza yameendelea tena leo sanjari na maroketi yanayovurumushwa na makundi yenye silaha ya Kipalestina kuelekea Israel, wakati wahudumu wa kibinadamu wa Umoja wa Mataifa wakiripoti kuuawa kwa watu zaidi ya 25,000 Gaza tangu kuanza kwa machafuko hayo mapya Oktoba 7 mwaka jana na mahitaji ya kibinadamu yakiongezeka kila uchao. 

Hali inazidi kubwa mbaya na hakuna dalili ya kukomesha uhasama Gaza limesema shirika la Umoja wa Mataifa la kuratibu misaada ya kibinadamu na masuala ya dharura OCHA. 

Sauti
2'22"