Mambo 10 lazima yatekelezwe kuleta afueni katika ukanda wa Gaza: Griffiths
Umoja wa Mataifa leo umesisitiza kwa mara nyingine kwamba kinachoendelea Gaza ni ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu huku kukiwa na ripoti kwamba vikosi vya Israel vimevamia Hospitali ya Al-Shifa jana usiku ambako mbali ya wagonjwa kuna maelfu ya raia waliotawanywa wanapata hifadhi na umeonya kwamba hospital sio uwanja wa vita na madhila hayo kwa raia wakiwemo watoto lazima yakome kwa kutekeleza mambo 10 ya muhimu.