Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari kwa Ujumla

UN News

Mambo 10 lazima yatekelezwe kuleta afueni katika ukanda wa Gaza: Griffiths

Umoja wa Mataifa leo umesisitiza kwa mara nyingine kwamba kinachoendelea Gaza ni ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu huku kukiwa na ripoti kwamba vikosi vya Israel vimevamia Hospitali ya Al-Shifa jana usiku ambako mbali ya wagonjwa kuna maelfu ya raia waliotawanywa wanapata hifadhi na umeonya kwamba hospital sio uwanja wa vita na madhila hayo kwa raia wakiwemo watoto lazima yakome kwa kutekeleza mambo 10 ya muhimu. 

Sauti
3'30"
© UNFPA/Bisan Ouda

Mfumo wa afya Gaza umeelemewa - Mashirika

Licha ya mashambulizi dhidi ya vituo vya afya na makazi ya watu katika Ukanda wa Gaza, mashirika mbalimbali ya Umoja wa Mataifa yanaendelea kujitahidi usiku na mchana kuhakikisha watu wanapata huduma ya afya ili kuokoa maisha yao lakini ni wazi kwamba hali inazidi kuwa mbaya kila uchao. Anold Kayanda amefuatilia suala hili na kutuandalia mada hii kwa kina. 

Sauti
4'2"
© UNICEF

Mtoto 1 kati ya 3 anakabiliwa na uhaba mkubwa wa maji - UNICEF

Mtoto mmoja kati ya Watoto watatu au saw ana watoto milioni 739 duniani kote - tayari wanaishi katika maeneo yaliyo na uhaba mkubwa au wa juu sana wa maji, na mabadiliko ya tabianchi yanatishia kufanya hali hii kuwa mbaya zaidi, imebainisha ripoti mpya ya shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Watoto UNICEF iliyotolewa usiku wa kuamkia leo Jumatatu kwa saa za New York, Marekani. 

Sauti
1'49"
UNICEF/NYHQ2014-1159/El Baba

Umoja wa Mataifa yaonya maisha ya watoto yanaendelea kupotea Gaza huku hali ya kukata tamaa ikitawala

Hali hatika hospitali za Gaza ni mbayá sana wagonjwa wakiendelea kupoteza maisha wakiwemo watoto njiti katika hospitali ya Al-Shifa ambayo kwa siku ya tatu mfululizo hakuna umeme huku mashambulizi ya Israel yakiongezeka, umesema Umoja wa Mataifa ambao leo unawaomboleza pia wafanyakazi wake 101 waliopoteza maisha katika mzozo huo na kusisitiza kwamba usitishwaji uhasama ni lazima sasa kuliko wakati mwingine wowote. 

Sauti
2'36"
UNSOM

Harakati za kujumuisha wanawake kwenye siasa Somalia zaendelea

Catriona Laing, Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Somalia amethibitisha kuwa Umoja wa Mataifa unashirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu na Wizara ya Maendeleo ya Wanawake na Haki za Binadamu nchini humo kuhakikisha kwamba sauti za wanawake zinasikika katika Baraza la Ushauri la Taifa (NCC) ambalo kwa sasa linaundwa na wanaume pekee akiwemo Rais wa shirikisho, marais wa majimbo na viongozi wengine wanaume wa ngazi ya juu ya uongozi.

Sauti
1'17"
© National Meteorological Centre, Libya

Machungu ya El Nino kuendelea hadi Aprili 2024 kaskazini na kusini mwa dunia

Tukio la mkondo joto la El Niño linalosababisha hivi sasa mvua kubwa, joto kali na ukame kwenye maeneo mbalimbali ya dunia, linatarajiwa kuendelea duniani na kuchochea ongezeko la kiwango cha joto baharini na ardhini, limesema shirika la Umoja wa Mataifa la Hali ya Hewa, WMO hii leo. Anold Kayanda na maelezo zaidi.

Taarifa ya WMO iliyotolewa leo mjini Geneva, Uswisi inaainisha kuwa El Nino ni mwenendo wa tabianchi unaoambatana na maji ya baharí kuwa ya joto kuliko kawaida kwenye maeneo ya mashariki mwa bahari ya Pasifiki na kusambaa maeneo mengine ya dunia.

Sauti
1'38"
UN News/ Hisae Kawamori

Kalavati 'lasogeza' huduma za afya kwa wanajamii Gambia

Nchini Gambia, Magharibi mwa bara la Afrika, kalavati au daraja dogo lililojengwa na shirika la Umoja wa Mataifa la maendeleo ya mitaji, UNCDF kwa ufadhili wa Muungano wa Ulaya (EU)ili kuunganisha maeneo mawili, Pakaliba na Baro Kunda, limesogeza huduma ya afya karibu na wakazi wa maeneo hayo. Anold Kayanda na maelezo zaidi

Sauti
1'30"
© UNICEF/Eyad El Baba

"Imetosha!" yasema mashirika ya kimataifa kwa kinachoendelea Gaza

Ikiwa ni siku 30 sasa tangu kuanza kwa mzozo huko Mashariki ya Kati, kati ya Israel na Wanamgambo wa Kipalestina wa Hamas walioko katika eneo la Palestina linalokaliwa kwa mabavu, Gaza, mashirika 18 ya Kimataifa ya misaada ya kibinadamu yametoa taarifa ya pamoja hii leo yakisema ‘imetosha’ wakitaka kusitishwa mara moja mzozo huo kwasababu za kibinadamu, mzozo ambao umegharimu maisha ya zaidi ya watu 10,000. Tupate taarifa zaidi kutoka kwa Leah Mushi.

Sauti
4'12"
UN

Ibara ya 12 ya UDHR inatekelezwa Tanzania?

Na sasa tuangazie Tamko la Umoja wa Mataifa la Haki za Binadamu ambalo mwaka huu linatimiza miaka 75. Na katika mfululizo wa vipindi vyetu vya kuelimisha umma kuhusu tamko hili kwa kuelezea Ibara kwa Ibara, ninakupeleka nchini Tanzania kwa mwanasheria na wakili Emmanuel Sosthenes kutoka shirika linalotoa msaada wa sheria kwa wanawake nchini humo, WILAC, akichambua Ibara ya 12 ya tamko hilo na jinsi inavyotekelezwa kwenye taifa hilo la Afrika Mashariki. Kwako Emmanuel. 


 

Sauti
2'11"
UN Photo/Albert Gonzalez Farran

Wanawake na wasichana wafungwa minyororo Sudan

Ofisi ya haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa (OHCHR) imesikitishwa sana na ripoti kwamba huko Darfur nchini Sudan wanawake na wasichana wanatekwa nyara na kushikiliwa katika mazingira ya yasiyo ya kiutu katika maeneo yanayodhibitiwa na wanamgambo waasi (RSF). Anold Kayanda na maelezo zaidi.  

Sauti
1'52"