Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari kwa Ujumla

IOM 2016/Amanda Nero

OHCHR linasema mashtaka yote dhidi ya waokoaji wa wahamiaji baharini huko Ugiriki yafutwe

Umoja wa Mataifa umeelezea wasiwasi wake kuhusu kesi iliyoanza huko Lesvos nchini Ugiriki dhidi ya watetezi 24 wa haki za binadamu wanaoshtakiwa kwa kutekeleza jukumu la kuokoa wahamiaji ambao walikumbwa na zahma baharini wakati wakikimbilia barani Ulaya kusaka maisha bora.

Msemaji wa Ofisi ya Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu haki za binadamu, Liz Throsell amewaambia waandishi wa habari mjini Geneva, Uswisi hii leo kuwa kesi za namna hiyo zinaharamisha kazi zinazookoa maisha na kuweka mwelekeo wa hatari. 

Sauti
2'12"
© UNICEF/Veronica Houser

Mradi uliofadhiliwa na TAKEDA, wawezesha Rwanda kuimarisha huduma kwenye hospitali na vituo vya afya: UNICEF

Nchini Rwanda, Umoja wa Mataifa unashirikiana na serikali kuimairisha huduma za uzazi ili hatimaye kuhakikisha kila uzazi unakuwa salama si tu kwa mama bali pia mtoto anayezaliwa. Kupitia mradi uliofadhiliwa na TAKEDA, kampuni hii ya utafiti na dawa duniani, Rwanda imeweza kuimarisha huduma kwenye hospitali na vituo vya afya.

Mradi huo wa ubia ulianza mwaka 2017. Wakati huo, Rwanda ndio ilikuwa imekamilisha malengo ya milenia, ikimaanisha baadhi ya malengo yalitimizwa, lakini kulikuwa na kusuasua katika baadhi ya maeneo mengine.

Sauti
7'2"
Picha: MONUSCO

Walinda amani wa UN kutoka Tanzania wafikisha misaada Hospitali ya Oicha, DRC

Kikosi cha 9, TANZBATT 9 cha wanajeshi walinda amani wa Umoja wa Mataifa kutoka Tanzania wanaohudumu nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC chini ya Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo DRC-MONUSCO, wameendelea na kampeni yao ya Afya na Amani ambapo hadi tarehe 13 mwezi huu wa Januari watakuwa wakiendelea kutoa misaada kwa jamii inayoishi katika eneo lao la kazi, kaskazini mashariki mwa nchi.

Walianza na Kituo cha afya cha Mavivi na sasa ilikuwa zamu ya Hospitali ya Oicha katika mji wa Beni jimboni Kivu Kaskazini.

Sauti
2'13"
WFP/Hugh Rutherford

WFP na GEP kwa kufanikisha mlo shuleni Burundi tayari inaonesha matokeo – UNICEF

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF linaripoti kuwa huduma ya chakula katika baadhi ya shule za msingi nchini Burundi tayari inaonesha matokeo chanya kuanzia mahudhurio shuleni na katika upande wa taaluma.

Burundi, nchi yenye udongo mzuri wenye rutuba ambayo kama si mabadiliko ya tabianchi kuathiri baadhi ya maeneo, changamoto ya kukosekana kwa chakula ingekuwa simulizi tu za kufikirika.

Sauti
1'45"
ILO

Ripoti mpya ya ILO imepigia chepuo mipango bunifu ya ufanyaji kazi kama ile iliyoanza kutumika wakati wa COVID-19

Ripoti mpya ya shirika la Umoja wa Mataifa la kazi duniani, ILO imepigia chepuo mipango bunifu ya ufanyaji kazi kama ile iliyoanza kutumika kufuatia mlipuko wa janga la COVID-19 ikisema inaweza kuleta manufaa kwa uchumi, biashara na wafanyakazi.

Ikipatiwa jina Mizania kati ya saa kazi na saa za kufurahia maisha duniani kote, ripoti imesema mipango hiyo inaweza kuongeza tija zaidi na mizania ya kazi na maisha yenye afya kwa mtumishi. 

Sauti
3'30"
Picha: MONUSCO

TANZBATT 9 waanzisha kampeni kutumia afya kuleta amani DRC

Kikosi cha tisa cha ulinzi wa amani kutoka Tanzania, TANZBATT 9 kinachohudumu ndani ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC Ujumbe wa Umoja wa Mataifa kulinda amani nchini DRC, MONUSCO, kimeanzisha kampeni iliyopewa jina la “Afya na Amani” ambayo inahusisha utoaji wa dawa za binadamu katika vituo vya Afya, Zahanati na Hospitali za baadhi ya maeneo ya uwajibikaji ya Kikosi hicho ndani ya mji wa Beni, kaskazini mashariki mwa DRC.

Sauti
5'37"
EQUIS Justicia para las mujeres/Scopio

Waliofungwa kwa kusimamia haki zao waachiliwe huru- Türk

Kufuatia kuanza kwa maadhimisho ya miaka 75 tangu kupitishwa kwa Tamko la Umoja wa Mataifa kuhusu haki za binadamu, UDHR, Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa haki za binadamu, Volker Türk ametoa wito kwa serikali duniani kote na mamlaka zote zinazoshikilia watuhumiwa kuwapatia msamaha au kuwaachilia huru wale wote walioswekwa ndani kwa kutekeleza haki zao za msingi.

Sauti
1'55"