OHCHR linasema mashtaka yote dhidi ya waokoaji wa wahamiaji baharini huko Ugiriki yafutwe
Umoja wa Mataifa umeelezea wasiwasi wake kuhusu kesi iliyoanza huko Lesvos nchini Ugiriki dhidi ya watetezi 24 wa haki za binadamu wanaoshtakiwa kwa kutekeleza jukumu la kuokoa wahamiaji ambao walikumbwa na zahma baharini wakati wakikimbilia barani Ulaya kusaka maisha bora.
Msemaji wa Ofisi ya Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu haki za binadamu, Liz Throsell amewaambia waandishi wa habari mjini Geneva, Uswisi hii leo kuwa kesi za namna hiyo zinaharamisha kazi zinazookoa maisha na kuweka mwelekeo wa hatari.