Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari kwa Ujumla

15 JANUARI 2020

Katika Jarida la Habari hii leo Grace Kaneiya anakuletea

-Ripoti mpya iliyotolea na shirika la Umoja wa Mataifa la idadi ya watu duniani UNFPA inasema hatua za haraka zinahitajika ili kunusuru maisha ya maelfu ya wanawake wajawaziti na watoto wanaozaliwa Darfur Magharibi baada ya kutawanywa na machafuko ya kikabila

-Msimu wa baridi umeelezwa kuongeza madhila zaidi kwa maelfu ya watu Idlib Syria hususan watoto kwa mujibu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF

Sauti
11'23"
OCHA/Giles

Benki ya Dunia na Ofisi ya Miradi ya UN washirikiana kuboresha maisha ya watu wa Yemen

Ofisi ya miradi ya Umoja wa Mataifa, UNOPS kwa kushirikiana na Benki ya dunia pamoja na wadau wenyeji, wanafanya juhudi za kuboresha huduma mijini pamoja na nishati ya umeme kwa mamilioni ya watu wa Yemen. Ni kufuatia miaka mitano ya vurugu nchini Yemen ambazo zimeharibu sana miundombinu na huduma za jamii zinazotegemewa sana na watu wa Yemen.

Sauti
1'58"