Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari kwa Ujumla

FAO na WFP kwa pamoja kukabiliana na njaa DRC

Mashirika mawili ya Umoja wa Mataifa, lile la chakula na kilimo FAO, na la mpango wa chakula WFP yamekusanya nguvu ili  kukabiliana na tatizo la njaa katika eneo la Kasai Kuu huko jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, DRC.

Alexis Bonte ambaye ni mwakilishi wa muda wa  FAO amesema watatumia kiasi cha dola milioni 10 zilizotolewa na serikali ya Ubelgiji ili kuboresha maisha ya raia laki moja ambao ni wakimbizi wa ndani katika migogoro ya wenyewe kwa wenyewe katika eneo la Kasai.

Azimio kuongeza misaada ya kibinadamu Syria lapitishwa

Hali mbaya ya kibinadamu inayoendelea kuighubika syria leo imetawala kikao cha baraza la usalama la Umoja wa Mataifa, ambapo maafisa wanaoshughulikia suala la kisiasa na kibinadamu nchini humo wametoa tarifa.

Mwakilishi maalumu wa Umoja wa Mataifa Syria Stefaffan de Mistura ametoa tarifa kuhusu  duru ya mwisho ya majadiliano iliyomalizika Geneva Uswis na kuwaleta pamoja wawakilishi wa serikali na upande wa upinzani. Hata hivyo amelalamikia ukweli kwamba hakuna mafanikio yoyote yaliyofikiwa katika mazungumzo hayo.

(SAUTI YA STAFFAN DE MISTURA)

Hali bado tete kwa wanawake na watoto CAR- UNICEF

Mwaka 2017 umekuwa ni mwaka mgumu zaidi kwa maisha ya wanawake na watoto nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR/

Hiyo ni kwa mujibu wa ripoti ya shirika la kuhudumia watoto duniani UNICEF, ikisema hakuna hata nuru kuwa hali itakuwa bora siku zijazo kutokana na hali ya usalama kuendelea kudorora.

Kwa mujbnu wa ripoti hiyo, vurugu na migogoro ya wenyewe kwa wenyewe inazidi kuongezeka  katika mikoa ya kaskazini magharibi na kuathiri maisha ya watu wengi ikiwemo  wanawake na watoto hivyo  kusababisha ukimbizi wa ndani.

Hebu fikiria maisha bila maji , kwa watoto wa Yemen hiyo ni kama ada

Ugonjwa wa kipindupindu na kuharisha umeongezeka mara dufu nchini Yemen mbali na zahma nyingine kama njaa, ukosefu wa mahitaji muhimu na mahangaiko ya vita kila uchao.

Mlipuko huo unatokana na uhaba mkubwa wa maji safi na salama vimesababishwa na kupanda kwa gharama za petroli nchini humo.

Mwakilishi wa shirika la Umoja wa Mataifa linalohudumia watoto UNICEF  Geert Cappelaere amesema  wanatoa lita 450, 000  za mafuta kila mwezi lakini kutokana na bei kuongezeka mara mbili zaidi ndani ya mwezi mmoja wamejikuta katika wakati mgumu.

Kutolinda suluhu ya mataifa mawili kunadhoofisha wasimamizi na kuimarisha wanamgambo:Mladenov

Umoja wa Mataifa umerejelea kauali yake kwamba Yerusalemu ni suala la mwisho kuhusu Mashariki ya Kati ambalo linapaswa kushughulikiwa kupitia mazungumzo ya amna kwa ana baina ya Israel na Palestina.

Hayo yamesemwa leo kwenye kikao cha baraza la Usalama na mratibu maalumu wa Umoja wa Mataifa kwa ajili ya mchakato wa mani ya Mashariki ya Kati Nikolai Mladenov alipotathimini ripoti ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu utekelezaji wa azimio namba 2334 kuanzia Septemba 20 hadi Desemba 18 mwaka huu.

Umoja wa Mataifa walaani shambulizi la msaafara wa misaada Nigeria

Mratibu wa shuguli za kibinadamu za Umoja wa Mataifa nchini Nigeria Bwana Edward Kallon amelaani vikali shambulizi la msafara wa misaada ya kibinadamu uliotokea tarehe 16 kazkazini mashariki mwa nchi hiyo.

Kwa mujibu wa taarifa hii, shambulizi  hilo lilitokea  katika mji wa Dikwa na Gamburu katika  jimbo la Borno na kusababisha vifo vya raia 4 na uharibifu mkubwa wa chakula kilichokua kinapelekwa kwa waathirika.