Ugonjwa wa kifua kikuu, changamoto na tiba
Kifua kikuu au TB!Gonjwa lililoorodheshwa na shirika la afya ulimwengni WHO kuwa miongoni mwa magonjwa 10 yanayoongoza kwa kusababisha vifo duniani.
WHO inasema mathalani mwaka 2015 watu milioni 10.4 waliugua ugonjwa huo, milioni 1.8 walifariki duniani, wakiwemo takribari watu Laki tano ambao walikuwa na virusi vya Ukimwi, VVU. Miongoni mwa waathirika ni kundi la wahamiaji ambalo katika maadhimisho ya siku ya kifua kikuu duniani tarehe 24 mwezi Machi, limeangaziwa.