Ushelisheli yajizatiti kulinda msingi wake wa uchumi
Pakua
Umoja wa Mataifa na washirika wake wamekuwa mstari wa mbele katika suala la mazingira kama ilivyo katika lengo namba 13 la ajenda ya maendeleo endelevu ya mwaka 2030 kuhusu mazingira na tabianchi. Katika mkutano wa Paris wa mwaka 2015, nchi wanachama walipitisha mkataba wa Paris wa mabadiliko ya tabianchi wenye lengo la kudhibiti shughuli za kiuchumi au kijamii zinazozalisha hewa ya ukaa, huku wakipigia chepuo utunzaji wa mazingira.Katika kutekeleza hilo nchi wanachama zinafanya kampeni za utunzaji bahari na viumbe wa baharini na leo tunaelekea katika visiwa vya Ushelisheli ambako Patrick Newman anakuletea makala kuhusu jitihada za serikali ya visiwa hivyo za kutunza bahari ambayo ni tegemeo kubwa kwa uchumi wan chi hiyo.