Vichwa vya Habari
Makala Maalum
Afya
Dkt. Natalia Kanem anapoangazia uongozi wake wa miaka minane katika shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ya Uzazi na Idadi ya Watu, (UNFPA), haanzi na takwimu za kimataifa, mafanikio ya mikutano, au hata kumbukumbu za ziara zake kwenye kambi za wakimbizi.
Habari kwa Picha
Taswira za utumikishaji watoto duniani
Tarehe 12 Juni ni siku ya kimataifa ya kupinga ajira kwa watoto. Tunamulika harakati za watoto za kujinasua kwenye umaskini kwa kutumikishwa ili mkono wao na familia zao uende kinywani.
Habari Nyinginezo
Haki za binadamu
Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) limetoa tamko likieleza masikitiko yake kufuatia vifo na taarifa za kukamatwa kwa watoto wakati wa maandamano ya Saba Saba yaliyoikumba Kenya mapema wiki hii. Taarifa hiyo, iliyotolewa kutoka ofisi ya UNICEF jijini Nairobi tarehe 9 Julai, imeangazia kifo cha msichana mdogo aliyepigwa risasi akiwa nyumbani kwao, tukio la kusikitisha ambalo limezua hasira kutoka kwa makundi ya kutetea haki na umma kwa ujumla.
Amani na Usalama
Chuo cha Mafunzo ya Ulinzi wa Amani Tanzania (TPTC), kwa kushirikiana na Umoja wa Mataifa (UN) kimezindua rasmi mafunzo ya ukufunzi kwa wanadhimu wa Umoja wa Mataifa. Mafunzo hayo yameanza tarehe 7 hadi 18 mwezi huu wa Julai katika chuo hicho kilichoko Dar es Salaam, nchini Tanzania.