Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UN News

Makala Maalum

Afya Dkt. Natalia Kanem anapoangazia uongozi wake wa miaka minane katika shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ya Uzazi na Idadi ya Watu, (UNFPA), haanzi na takwimu za kimataifa, mafanikio ya mikutano, au hata kumbukumbu za ziara zake kwenye kambi za wakimbizi.

Habari Nyinginezo

Haki za binadamu Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) limetoa tamko likieleza masikitiko yake kufuatia vifo na taarifa za kukamatwa kwa watoto wakati wa maandamano ya Saba Saba yaliyoikumba Kenya mapema wiki hii. Taarifa hiyo, iliyotolewa kutoka ofisi ya UNICEF jijini Nairobi tarehe 9 Julai, imeangazia kifo cha msichana mdogo aliyepigwa risasi akiwa nyumbani kwao, tukio la kusikitisha ambalo limezua hasira kutoka kwa makundi ya kutetea haki na umma kwa ujumla.
Amani na Usalama Chuo cha Mafunzo ya Ulinzi wa Amani Tanzania (TPTC), kwa kushirikiana na Umoja wa Mataifa (UN) kimezindua rasmi mafunzo ya ukufunzi kwa wanadhimu wa Umoja wa Mataifa. Mafunzo hayo yameanza tarehe 7 hadi 18 mwezi huu wa Julai  katika chuo hicho kilichoko Dar es Salaam, nchini Tanzania.