Chaguo la Mhariri
Makala Maalum
Haki za binadamu
Hali katika vituo vya rumande nchini Ufilipino, ambayo imeelezwa kuwa “si ya kibinadamu” na mmoja wa majaji wa mahakama ya juu nchini humo, inatarajiwa kuboreka kwa kasi wakati taifa hilo la Kusini Mashariki mwa Asia likielekea katika kupitisha sheria zinazozingatia haki za binadamu na utu wa wafungwa na kupendekeza kiwango cha chini cha matibabu katika vituo vyote vya rumande.
Habari kwa Picha
Harakati za kusaka usalama huko Gaza
Wengi wa wananchi wa Gaza milioni 2.3 wanakimbia ghasia zinazozidi kaskazini na Kusini mwa Gaza kutokana na vita ambayo sasa ina miezi saba na ambayo imesababisha vifo vya wapalestina 36,000 na kuwaacha wengine katika njaa huku wengine wakiwa wamefukiwa kwenye vifusi katika maeneo yaliyo zingirwa.
Habari Nyinginezo
Tabianchi na mazingira
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres leo ametoa wito wa dharura wa kuchukua hatua ili kulinda vyema mabilioni ya watu duniani kote walioathiriwa na athari za joto kali, huku ongezeko la joto duniani likiendelea kupanda bila dalili ya kupungua.
Msaada wa Kibinadamu
Wakati Rais wa Marekani Joe Biden akijiandaa kukutana na waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu hii leo nchini Marekani ambapo wanatarajia kujadili maendeleo ya kusitisha mapigano huko Ukanda wa Gaza na kuachiliwa kwa mateka wote ambao bado wanashikiliwa katika eneo hilo, hali ya njaa na utapiamlo imeendelea kuwakumba Wanagaza, huku mashirika ya kibinadamu wa Umoja wa Mataifa yakionya kwamba hakuna kilimo cha eneo kubwa wala bustani kinachofanyika sabab ya ukosefu wa usalama.