Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UN News

Makala Maalum

Haki za binadamu Hali katika vituo vya rumande nchini Ufilipino, ambayo imeelezwa kuwa “si ya kibinadamu” na mmoja wa majaji wa mahakama ya juu nchini humo, inatarajiwa kuboreka kwa kasi wakati taifa hilo la Kusini Mashariki mwa Asia likielekea katika kupitisha sheria zinazozingatia haki za binadamu na utu wa wafungwa na kupendekeza kiwango cha chini cha matibabu katika vituo vyote vya rumande.

Habari Nyinginezo

Tabianchi na mazingira Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres leo ametoa wito wa dharura wa kuchukua hatua ili kulinda vyema mabilioni ya watu duniani kote walioathiriwa na athari za joto kali, huku ongezeko la joto duniani likiendelea kupanda bila dalili ya kupungua.
Msaada wa Kibinadamu Wakati Rais wa Marekani Joe Biden akijiandaa kukutana na waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu hii leo nchini Marekani ambapo wanatarajia kujadili maendeleo ya kusitisha mapigano huko Ukanda wa Gaza na kuachiliwa kwa mateka wote ambao bado wanashikiliwa katika eneo hilo, hali ya njaa na utapiamlo imeendelea kuwakumba Wanagaza, huku mashirika ya kibinadamu wa Umoja wa Mataifa yakionya kwamba hakuna kilimo cha eneo kubwa wala bustani kinachofanyika sabab ya ukosefu wa usalama.