Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Kauli za chuki zinasababisha mauaji ya kimbari - Alice Wairimu Nderitu

Kauli za chuki zinasababisha mauaji ya kimbari - Alice Wairimu Nderitu

Pakua

Leo siku ya kimataifa ya kupinga kauli za chuki ikiadhimishwa ambayo mwaka huu imebeba maudhui “Nguvu ya Vijana ya Kupinga na Kushughulikia Kauli za Chuki”, Dunia bado iko katika kumbukumbu za maombolezo ya siku 100 za mauaji ya Kimbari ya Rwanda yaliyofanyika miaka 30 iliyopita, ambapo kauli za chuki zimeelezwa kuwa moja ya chachu kubwa ya mauaji hayo. Flora Nducha wa Idhaa hii ameketi na Alice Wairimu Nderitu mshauri maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu kuzuia mauaji ya kimbali kujadili kuhusu mchango wa kauli za chuki katika zahma duniani, jukumu la vijana na nini kifanye kuzitokomeza. Na Bi. Nderitu anaanza kwa kufafanua je dunia inaelewa kuhusu mchango wa kauli hizo za chuki katika mauaji ya kimbari.

Audio Credit
Assumpta Massoi/Flora Nducha
Audio Duration
7'53"
Photo Credit
UN News/Assumpta Massoi