Leo ni siku ya ukungu duniani
Kwa mara ya kwanza dunia leo inaadhimisha siku ya ukungu ili kukumbuka watu waliopoteza maisha kutokana na athari za ukungu.
Maadhimisho haya yanafanyika ikiwa ni siku ya pili ya mkutano mkuu wa baraza la shirika la mazingira la Umoja wa Mataifa, UNEA huko Nairobi, Kenya.
Imeelezwa kuwa binadamu katika uhai wake ana vitu vingine anavyoweza kutumia au la lakini si hewa ambayo anahitaji wakati wote wa uhai wake.
Umoja wa Mataifa unasema kwa wastani kila binadamu anahitaji galoni milioni 250 za hewa katika mapafu yake ikiwa ni sawa na galoni elfu 10 za hewa kwa siku.
Mathalani ukungu kutanda hewani wanashindwa kupumua au kuona vizuri
Mohammed Tariq dereva Bajaj jijini New Delhi, India ameeleza madhila anayokumbana nayo akiwa kazini hususan hewa chafu itokayo kwenye magari na kueleza hana namna ya kujikinga nayo na lazima afanye biashara