Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

USA

Watoto wa kike wang’ara utafiti wa kujua kusoma- UNESCO

Zaidi ya asilimia 96 ya watoto wenye umri wa miaka ya kati ya 9 hadi 10 wanajua kusoma

Ripoti ya utafiti wa zaidi ya nchi 50 duniani uliofanywa na shirika la Umoja wa Mataifa la elimu, sayansi na utamaduni, UNESCO umeonyesha kuwa watoto wa kike wanaongoza zaidi kuliko wa kiume.

Nchi ya Urusi imeongoza katika utafiti huo ikifuatiwa na Singapore, Hong Kong, Ireland, Finland na Poland.

Leo ni siku ya ukungu duniani

Kwa mara ya kwanza dunia leo inaadhimisha siku ya ukungu ili kukumbuka watu waliopoteza maisha kutokana na athari za ukungu.

Maadhimisho haya yanafanyika ikiwa ni siku ya pili ya mkutano mkuu wa baraza la shirika la mazingira la Umoja wa Mataifa, UNEA  huko Nairobi, Kenya.

Imeelezwa kuwa binadamu katika uhai wake ana vitu vingine anavyoweza kutumia au la lakini si hewa ambayo anahitaji wakati wote wa uhai wake.

WHO yatoa msaada wa vifaa vya tiba Libya

Shirika la afya duniani  WHO limetoa msaada wa mitambo ya kusaidia kupumua kwa wangonjwa mahututi katika hospitali ya Tragen kusini mwa Libya

Msaada huo wa mitambo miwili pamoja na vipuri vyake vyote umetolewa kufuatia kuwepo na upungufu mkubwa wa vifaa hivyo vya tiba kwa wagonjwa mahututi na wenye kuhitaji usaidizi wa kupumua.

WHO imeeleza kujizatiti kuendelea kutoa msaada wa kibinadamu kwenye nyanja ya afya maeneo yote nchini Libya .

Fedha za kununulia vifaa tiba hivyo zimetoka kwenye mfuko wa dharura wa Umoja wa Mataifa CERF

Saidieni kupambana na uharibifu wa mazingira: Guterres

Tuna haki ya kuishi sehemu salama, tunategemea kula chakula bora, maji safi na kuvuta hewa safi lakini bado tunaendelea kuharibu mazingira.

Huo ni ujumbe wa Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres katika mkutano mkuu wa shirika la mazingira la Umoja wa Mataifa unaofanyika Nairobi, Kenya.

Guterres amesema tayari kuna mbinu na maazimio madhubuti za kupambana na mabadiliko ya tabia nchi yanayoweza kuigwa kuinusuru dunia isiendelee kuathirika.