Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

London

14 MACHI 2023

Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ambapo katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa mkutano wa 67 wa hali ya wanawake duniani, CSW67 ukiendelea maudhui yakiwa nafasi ya teknolojia na ugunduzi katika kumsongesha mwanamke tunapata mgeni studio ambaye ni John Nyirenda, kijana huyu, Muasisi na Mkurugenzi Mtendaji wa shirika lisilo la kiserikali la kusongesha ustawi wa vijana nchini Malawi, YouthWAVE Malawi. Pia tunakuletea habari kwa ufupi za UNIDO, WHO na AFSD. Mashinani tutaelekea nchini Ethiopia, kulikoni?.

Sauti
13'18"

Leo ni siku ya ukungu duniani

Kwa mara ya kwanza dunia leo inaadhimisha siku ya ukungu ili kukumbuka watu waliopoteza maisha kutokana na athari za ukungu.

Maadhimisho haya yanafanyika ikiwa ni siku ya pili ya mkutano mkuu wa baraza la shirika la mazingira la Umoja wa Mataifa, UNEA  huko Nairobi, Kenya.

Imeelezwa kuwa binadamu katika uhai wake ana vitu vingine anavyoweza kutumia au la lakini si hewa ambayo anahitaji wakati wote wa uhai wake.

FAO yapigia chepuo elimu ya kilimo cha chakula

Mkurugenzi Mkuu wa shirika la chakula na kilimo duniani Jose Graziano da Silva amesema elimu juu ya kilimo cha mazao ya chakula ndio njia mpya inayopaswa kufuatwa na nchi zote duniani katika kujihakikisha uwepo wa chakula cha kutosha na kitakachopatikana kwa uendelevu.

Bwana Graziano da Silva ameyasema hayo katika mkutano wa viongozi waandamizi wa shirika hilo huko mjini London, Uingereza.