Mameya kutoka miji 50 duniani wakutana London kujadili NCDs na majeraha: WHO
Shirika la Umoja wa Mataifa la afya duniani WHO limesema mameya na maafisa wengine kutoka zaidi ya miji 50 kote duniani wanakutana London Uingereza kuanzia leo Machi 14 hadi Machi 16 kushughilikia magonjwa yasio ya kuambukiza NCDs na kuzuia majeraha, katika mkutano wa kwanza wa ushirikiano kwa ajili ya miji yenye afya.