Malawi: Hali ya chakula ni tete, WFP yaomba jamii ya kimataifa ichukue hatua
Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula duniani, WFP linatoa wito wa upelekaji wa haraka wa misaada ya chakula kwa ajili ya kuokoa maisha kwa watu milioni mbili wanaokabiliwa na njaa iliyochochewa na ukame. Ukame umesababishwa na hali ya El Niño.