Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Kenya kuunda viashirio vipya vya kupima usawa wa kijinsia katika sekta ya biashara.
UNCTAD

UNCTAD/UNECA: Kenya kuunda viashirio vipya vya kupima usawa wa kijinsia katika sekta ya biashara.

Umoja wa Mataifa umekuwa ukipigia upatu lengo namba tano la Malengo Endelevu ya Umoja huo linalohimiza usawa kwa wote katika nyanja zote ifikapo mwaka 2030. Hata hivyo ili kuelewa jinsi biashara inavyoathiri wanaume na wanawake ni muhimu kuunda sera za biashara zinazojumuisha zaidi na zenye usawa ambazo zinakuza usawa wa kijinsia na uwezeshaji wa kiuchumi kwa wote,hii inahitaji takwimu nzuri za kitaifa kuhusu jinsia katika biashara.

Sauti
3'8"
Hapa ni Beni, jimboni Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, walinda amani wa Umoja wa Mataifa kutoka Brazil wanaohudumu kikosi cha kujibu mashambulizi FIB cha MONUSCO wakipatia mafunzo wanajeshi 30 kutoka jeshi la serikali, FARDC j…
MONUSCO/Ado Abdou

DRC: MONUSCO yapatia wanajeshi 30 wa FARDC mbinu za kukabili waasi msituni

Siku zikizidi kuhesabiwa kwa Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, MONUSCO, kuondoka nchini humo, ujumbe huo unaendelea kutekeleza wajibu wake wa kujengea uwezo jeshi la serikali, FARDC kuweza kukabili vikundi vilivyojihami ambavyo vinatajwa kuhusika na asilimia 65 ya matukio ya ukiukwaji wa haki za binadamu nchini humo mwezi Februari mwaka huu, kwa mujibu wa ripoti ya pamoja ya Umoja wa Mataifa na serikali. 

Sauti
2'12"
Msaada wa chakula unaotolewa na World Central Kitchen ukipangwa kwenye boti inayoondoka Italia. (Maktaba)
© Open Arms

Gaza: UN yalaani vikali mauaji ya wahudumu 7 wa misaada ya kibinadamu

Leo maafisa wa masuala ya kibinadamu wa Umoja wa Mataifa wamelaani vikali mauaji ya wafanyakazi wa misaada 7 wa shirika lisilo la kiselikali au NGO la World Central Kitchen yaliyofanywa na jeshi la Israel, maafisa hao wakirejea kueleza hofu yao kwamba hakuna mahali palipo salia kuwa salama Gaza. Akizungumzia mauaji hayo Jamie McGoldrick, Mratibu wa masuala ya kibinadamu katika eneo linalokaliwa la Palestina amesema “Hili sio tukio la kipekee kwani hadi kufikia Machi 20 wahudumu wa kibinadamu 196 wameuawa Gaza tangu Oktoba 7 mwaka jana na hii ikiwa ni karibu mara tatu zaidi ya idadi ya vifo iliyorekodiwa katika mgogoro mmoja kwa mwaka."