Shambulizi dhidi ya walinda amani DRC, UN yalaani
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres amelaani shambulizi ambalo limetokea jana Jumamosi Machi 16 na kujeruhi wanajeshi wanane wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, wakati wa mapigano kati ya waasi wenye nguvu wa M23 na wanajeshi wa Serikali.