Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Helikopta za MONUSCO zikizunguka Ituri DRC (Kutoka Maktaba)
MONUSCO/Nazar Voloshyn

Shambulizi dhidi ya walinda amani DRC, UN yalaani

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres amelaani shambulizi ambalo limetokea jana Jumamosi Machi 16 na kujeruhi wanajeshi wanane wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, wakati wa mapigano kati ya waasi wenye nguvu wa M23 na wanajeshi wa Serikali.

Kamanda wa TANZBATT-10, Luteni Kanali John Peter Kalabaka akimkabidhi bendera ya Tanzania Luteni Kanali  Vedasto Ernest Kikoti ikiwa ni ishara ya kukabidhiana majukumu ya ulinzi wa amani huko Beni Mavivi jimboni Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokra…
TANZBATT-10

Wananchi DRC eleweni na ikubalini dhamira ya UN ya kulinda raia - TANZBATT-11

Hii leo huko jimboni Kivu Kaskazini mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, kikosi cha 10 cha Tanzania (TANZBATT-10)  kilichoko kwenye brigedi ya mapigano (FIB) ya ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, MONUSCO imekabidhi majukumu kwa kikosi cha 11, TANZBATT-11, katika hafla iliyofanyika eneo la Beni-Mavivi. Msimulizi wetu ni Kapteni Abubakari Muna, Afisa Habari wa TANZBATT-10.

Sauti
3'28"
Pamela Achieng, Hakimu katika mahakama ya Ngong iliyo katika Kaunti ya Kajiado nchini Kenya.
UN News

Wasichana ni majaji watarajiwa, wafuate ndoto zao jamii ziendelee kunufaika - Hakimu Pamela Achieng

Mkutano wa 68 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake duniani, CSW68 ukiendelea hapa jijini New York Marekani tunavinjari hadi nchini Kenya kumsikia Hakimu Pamela Achieng ambaye azma yake ya kujikita kwenye masula ya kusimamia haki ilichochewa na swali alilojiuliza yeye mwenye ya kwamba  “kama mwanaume anaweza kufanya kazi zinazotambulika hasa za kutetea haki za raia katika mahakama kwanini mwanamke asiweze?”

 

 

Sauti
6'16"
Jill Lawler, Mkuu wa Operesheni za Mashinani na Dharura wa shirika la Umoja wa MAtaifa la kuhudumia watoto UNICEF, nchini Sudan akiwa ziarani Khartoum.
© UNICEF

Sudan: Watu 300 wakatwa miguu mwezi mmoja uliopita pekee

Miezi 11 ya vita nchini Sudan imesababisha machungu kwa watoto na vijana ambako ujumbe wa hivi karibuni wa shirika moja la Umoja wa Mataifa uliozuru hospitali kwenye mji mkuu Khartoum umeshuhudiwa vijana waliokatwa miguu, huku Mkurugenzi wa hospitali hiyo akisema mwezi mmoja uliopita pekee watu wapatao 300 walikatwa miguu yao kutokana na madhara ya vita.

Watoto katika makazi ya Muda Gaza
© UNRWA

Gaza: Tutaendea vipi na usaidizi kiwa misaada kila wakati iko kwenye tishio? – Mkuu wa OCHA

Kukiwa na ripoti za kwamba leo Wapalestina 6 wameuawa kwa kupigwa risasi na wengine 83 wakijeruhiwa wakati wakisubiri malori ya misaada huko Gaza, Mkuu wa Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kuratibu misaada ya kibinadamu OCHA, Martin Griffiths kupitia ukurasa wa mtandao wa X ametoa wito wa kulindwa kwa operesheni za misaada ya kibinadamu inayohitajika sana Gaza.