Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Kila mwaka, mamilioni ya wasichana na wavulana kote ulimwenguni wanakabiliwa na unyanyasaji wa kijinsia na udhalilishaji.
© UNICEF/Estey

Biashara na unyanyasaji wa kingono wa watoto ukomeshwe kwenye vyombo vya habari na tasnia ya burudani

Hii leo huko jijini Geneva Uswisi mkutano wa 55 wa Baraza La Umoja wa Mataifa la Haki za Binadamu umeendelea ambapo Mtaalamu wa Umoja wa Mataifa kuhusu biashara na unyanyasaji wa kingono wa watoto Mama Fatima Singhateh ametaka kutambulika kwa hatua za mtu mmoja mmoja au za pamoja za kupambana na unyanyasaji wa kijinsia na unyonyaji wa watoto katika tasnia ya burudani na vyombo vya habari ili kukomeshwa unyanyasiji huo mara moja.

Pramila Patten, Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Ukatili wa Kingono kwenye mizozo, akihutubia waandishi wa habari katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa, New York.
UN Photo/Mark Garten

Mwakilishi Maalum wa UN: Kuna 'Taarifa za wazi na zenye kushawishi' kwamba mateka wanaoshikiliwa Gaza walifanyiwa ukatili wa kingono

Kufuatia ziara ya siku 17 nchini Israel, Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Ukatili wa Kingono kwenye mizozo Pramila Patten ameripoti hii leo kwamba yeye na timu ya wataalam wamekuta "taarifa za wazi na za kushawishi" za ubakaji, na mateso ya kijinsia yaliyofanywa dhidi ya mateka waliokamatwa wakati wa mashambulio ya kigaidi ya Oktoba 7, 2023 huko Israel.