Biashara na unyanyasaji wa kingono wa watoto ukomeshwe kwenye vyombo vya habari na tasnia ya burudani
Hii leo huko jijini Geneva Uswisi mkutano wa 55 wa Baraza La Umoja wa Mataifa la Haki za Binadamu umeendelea ambapo Mtaalamu wa Umoja wa Mataifa kuhusu biashara na unyanyasaji wa kingono wa watoto Mama Fatima Singhateh ametaka kutambulika kwa hatua za mtu mmoja mmoja au za pamoja za kupambana na unyanyasaji wa kijinsia na unyonyaji wa watoto katika tasnia ya burudani na vyombo vya habari ili kukomeshwa unyanyasiji huo mara moja.