Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Mtaalamu Maalum wa Umoja wa Mataifa anayeshughulika na masuala ya mateso, na Adhabu nyingine za Kikatili, za Kinyume cha utu au za Kushusha hadhi, Alice Jill Edwards.
UN Video

Wataalamu wa UN wapinga utekelezaji wa hukumu ya kifo kwa kutumia gesi ya nitrojeni hypoxia

Wataalamu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa akiwemo Alice Jill Edwards, anayeshughulikia masuala yanayohusu mateso, na Adhabu nyingine za Kikatili, za Kinyama au ya Kushusha, hadhi leo Januari 3 mjini Geneva-Uswisi wameelezea wasiwasi wao kuhusu kukaribia kutekelezwa kwa hukumu ya kifo kwa kutumia gesi ya nitrojeni hypoxia dhidi ya Kenneth Eugene Smith hapa nchini Marekani.  

Sauti
2'1"
Mtoto mwenye umri wa miaka minane akisubiri mgao wa chakula huko Rafah, kusini mwa Gaza
© UNICEF/Abed Zagout

GAZA: Mashambulizi yakishamiri, njaa na magonjwa navyo vyatawala

Mashirika ya Umoja wa Mataifa ya usaidizi wa kiutu hii leo Jumanne yameendelea kuelezea wasiwasi wao mkubwa juu ya hatma ya raia walionasa kwenye mapigano huko Ukanda wa Gaza wakati huu kukiwa na ripoti ya kwamba jeshi la Israel limeendelea na mashambulizi kwenye miji ya kusin mwa Gaza ya Deir al Balah, Khan Younis na Rafah huku vikundi vya kipalestina vilivyojihami vikirusha makombora usiku kucha kuelekea Israel.