Nimesikitishwa tulishindwa kulinda watumishi wetu Gaza – Guterres
Hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa leo kumefanyika tukio la kila mwaka la kukumbuka wafanyakazi 188 wa chombo hicho waliouawa mwaka 2023 pekee wakiwemo 135 watumishi wa UNRWA waliouawa ukanda wa Gaza kufuatia mashambulizi yaliyoanza Oktoba 7, 2023 baada ya wanamgambo wa Hamas kushambulia Israeli na ndipo Israeli ikaanza kujibu mashambulizi hadi leo hii.