UNESCO yahimiza matumizi ya lugha mama kwenye ufundishaji
Tarehe 21 Februari kila mwaka ulimwengu unaadhimisha siku ya lugha mama ambayo mwaka huu Kali mbiu yake ni “Elimu ya Lugha nyingi ni nguzo ya kujifunza kati ya vizazi.”
Tarehe 21 Februari kila mwaka ulimwengu unaadhimisha siku ya lugha mama ambayo mwaka huu Kali mbiu yake ni “Elimu ya Lugha nyingi ni nguzo ya kujifunza kati ya vizazi.”
Umoja wa Mataifa umesema Ukraine sasa ni moja ya nchi zilizoathiriwa zaidi na mabomu ya kutegwa ardhini duniani huku ikadiriwa kwamba karibu thuluthi moja ya nchi hiyo imeghubikwa na vita eneo ambalo ukubwa wake ni mara nne na nusu ya nchi ya Uswisi. Umoja wa Mataifa umekuwa ukifanya kazi na serikali ya Ukraine kwa miaka 30 na umekuwa ukiongoza mpango wa utekelezaji wa uteguaji wa mabomu ya kutegwa ardhini tangu 2016.
Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, Bintou Keita, ameliambia Baraza la Usalama kwamba ana wasiwasi mkubwa kutokana na ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu na sheria za kimataifa unaofanywa katika maeneo yaliyo chini ya udhibiti wa M23, ambapo vuguvugu hilo linalenga watendaji wa mashirika ya kiraia, hasa watetezi wa haki za binadamu na waandishi wa habari.
Mapigano kati ya M23 na wanajeshi wa Congo (FARDC) yameongezeka katika maeneo kadhaa na "M23 imepanua mipaka yake zaidi kusini, na kusababisha kuhama zaidi kwa watu kuelekea Goma na Kivu Kusini.” Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC ambaye pia ni Mkuu MONUSCO, Bintou Keita, amesema leo.
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limekutana leo mjini New York kuhusu Gaza ambapo Marekani imeamua kutumia kura yake ya turufu kupinga azimio lililotolewa kwa niaba ya mataifa ya Kiarabu na Algeria likitaka "kusitishwa mara moja kwa mapigano Gaza kwa minajili ya kibinadamu ambalo lazima yaheshimiwe na pande zote".
Umoja wa Mataifa umetenga dola za Marekani milioni 100 ili kusaidia kwenye majanga ya kibinadamu yenye ufadhili mdogo zaidi duniani.
Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na jumuiya ya misaada ya kibinadamu leo wamezindua ombi la dola bilioni 2.6 za kimarekani ili kufadhili mpango wa misaada ya kibinadamu wa mwaka huu wa 2024 nchini humo.
Hali ya kibinadamu Gaza na hasa Kusini mwa Ukanda huo ambako zaidi ya watu milioni 1 wanapata hifadhi inaendelea kuwa mbayá yameonya leo mashirika ya Umoja wa Mataifa.
Mkataba wa marufuku ya biashara ya pembe za faru inayotekelezwa kupitia mkataba wa kuwalinda wanyamapori walio katika hatari ya kutoweka, CITIES, umepata msukumo mpya.
Kabla ya kusikilizwa kwa kesi iliyopangwa ya Julian Assange nchini Uingereza, ambako kuna uwezekano mkubwa atarejeshwa Marekani kwa lazima, mtaalam huru wa Umoja wa Mataifa ameelezea wasiwasi wake kuhusu uwezekano wa ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu dhidi ya mwanzilishi huyo wa WikiLeaks, akionya zaidi kwamba kuanathari za kesi hiyo zinaweza kuathiri kwa kiasi kikubwa uandishi wa habari duniani na uhuru wa kujieleza.