Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

UNDP inasaidia kutegua mabomu ya ardhini nchini Ukraine.
UNDP in Ukraine/Alexander Ratushnyak

Uondoaji wa mabomu ya kutengwa ardhini Ukraine ni mtihani na hatari kubwa: Paul Heslop

Umoja wa Mataifa umesema Ukraine sasa ni moja ya nchi zilizoathiriwa zaidi na mabomu ya kutegwa ardhini duniani huku ikadiriwa kwamba karibu thuluthi moja ya nchi hiyo imeghubikwa na vita eneo ambalo ukubwa wake ni mara nne na nusu ya nchi ya Uswisi. Umoja wa Mataifa umekuwa ukifanya kazi na serikali ya Ukraine kwa miaka 30 na umekuwa ukiongoza mpango wa utekelezaji wa uteguaji wa mabomu ya kutegwa ardhini tangu 2016. 

Sauti
2'33"
Wapiganaji wa M23 wakielekea Goma DRC, (Kutoka Maktaba)
© MONUSCO/Sylvain Liechti

Nina wasiwasi mkubwa na ukikukwaji wa haki za binadamu katika maeneo yanayokaliwa na M23 – Bintou Keita

Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, Bintou Keita, ameliambia Baraza la Usalama kwamba ana wasiwasi mkubwa kutokana na ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu na sheria za kimataifa unaofanywa katika maeneo yaliyo chini ya udhibiti wa M23, ambapo vuguvugu hilo linalenga watendaji wa mashirika ya kiraia, hasa watetezi wa haki za binadamu na waandishi wa habari.

Sauti
2'10"
Bintou Keita (kwenye skrini), Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa UN na Mkuu wa Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa Kulinda Amani DRC, akitoa maelezo kwa mkutano wa Baraza la Usalama kuhusu hali inayoihusu nchi hiyo.
UN Photo/Loey Felipe

Mwakilishi wa UN DR Congo aeleza Baraza la Usalama hali  inavyozidi kuwa tete

Mapigano kati ya M23 na wanajeshi wa Congo (FARDC) yameongezeka katika maeneo kadhaa na "M23 imepanua mipaka yake zaidi kusini, na kusababisha kuhama zaidi kwa watu kuelekea Goma na Kivu Kusini.” Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC ambaye pia ni Mkuu MONUSCO, Bintou Keita, amesema leo. 

Julian Assange akizungumza na vyombo vya habari mjini London Uingereza (Kutoka Maktaba)
© Foreign Ministry of Ecuador/David G. Silvers

MAHOJIANO: Mtaalamu huru wa UN anaonya juu ya athari za kumuhamishia Assange Marekani

Kabla ya kusikilizwa kwa kesi iliyopangwa ya Julian Assange nchini Uingereza, ambako kuna uwezekano mkubwa atarejeshwa Marekani kwa lazima, mtaalam huru wa Umoja wa Mataifa ameelezea wasiwasi wake kuhusu uwezekano wa ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu dhidi ya mwanzilishi huyo wa WikiLeaks, akionya zaidi kwamba kuanathari za kesi hiyo zinaweza kuathiri kwa kiasi kikubwa uandishi wa habari duniani na uhuru wa kujieleza.