Habari kwa ufupi: Mauaji ya mlinda amani CAR; Kipindupindu; Matumizi ya tumbaku
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amelaani mauaji ya jana Januari 15 ambapo aliuawa mlinda amani mmoja wa kutoka Cameroon aliyekuwa anahudumu katika Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa Kulinda amani nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati (MINUSCA) na kujeruhiwa kwa watu wengine watano, wawili kati yao wakiwa wamejeruhiwa mno kutokana na mlipuko huko Mbindali, katika Mkoa wa Ouham-Pendé, kaskazini-magharibi mwa Paoua.