Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

UN Photo/Catianne Tijerina
UN Photo/Catianne Tijerina

Habari kwa ufupi: Mauaji ya mlinda amani CAR; Kipindupindu; Matumizi ya tumbaku

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amelaani mauaji ya jana Januari 15 ambapo aliuawa mlinda amani mmoja wa kutoka Cameroon aliyekuwa anahudumu katika Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa Kulinda amani nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati (MINUSCA) na kujeruhiwa kwa watu wengine watano, wawili kati yao wakiwa wamejeruhiwa mno kutokana na mlipuko huko Mbindali, katika Mkoa wa Ouham-Pendé, kaskazini-magharibi mwa Paoua. 

Profesa Celeste Saulo, Katibu Mkuu mpya wa shirika la Umoja wa Maytaifa la utabiri wa hali ya hewa duniani WMO
UNOG/Srdjan Slavkovic

Mifumo bora ya tahadhari ya mapema ya majanga ni kipaumbele cha WMO: Celeste Saulo

Katibu Mkuu mpya wa shirika la Umoja wa Maytaifa la utabiri wa hali ya hewa duniani WMO Profesa Celeste Saulo amesema kuimarisha mifumo ya tahadhari ya mapema ambayo inafuatilia wakati na lini majanga yanapotokea ni kipaumbele muhimu katika uongozi wake a,mbacho kitasaidia kupunguza hatari ya majanga ya asili ambayo yanachochewa na mabadiliko ya tabianchi.

Watoto wakisubiri kugawiwa chakula huko Rafah, kusini mwa Ukanda wa Gaza.
© UNICEF/Abed Zagout

Siku 100 za mzozo: Hatuwezi kuruhusu yanayotokea Gaza kuendelea, wala kutokea Lebanon - Guterres

Siku 100 tangu kuanza kwa mzozo wa Israel na Palestina, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres leo Januari 15 akizungumza na wanahabari jijini New York Manreakni ametaka "kuachiliwa mara moja na bila masharti kwa mateka wote. "Pia akiongeza kusema mashambulizi dhidi ya Gaza yaliyotekelezwa na vikosi vya Israeli katika siku hizi 100 yamesababisha uharibifu mkubwa na viwango vya mauaji ya raia kwa kiwango ambacho hakijawahi kutokea katika miaka ya uongozi wake kama Katibu Mkuu."

Mashirikak ya UN na wadau wake wanatoa misaada kwa watu walioathiriwa na mapigano mapya huko Lviv
© UNOCHA/Allaham Musab

UN yazindua ombi la dola bilioni 4.2 kwa ajili ya kuwasaidia Waukraine

Takriban miaka miwili sasa tangu majeshi ya Urusi yaanzishe "vita kamili na kuikalia Ukraine, amesema leo mkuu wa Umoja wa Mataifa wa misaada ya kibinadamu na masuala ya dharura Martin Griffiths akitoa ombi la dharura la pamoja na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR la dola bilioni 4.2 ili kuwasaidia walio hatarini nchini Ukraine.

Malori yaliyosheheni msaada wa kibinadamu yakijiandaa kuingia Gaza kupitia kivuko cha Rafah
© UNICEF/Eyad El Baba

Mashirika ya UN yaomba kufunguliwe njia nyingine ya kufikisha misaada Gaza

Zikiwa ni zaidi ya siku 100 tangu kuibuka upya kwa mzozo huko Mashariki ya Kati, mashirika ya Umoja wa Mataifa hii leo yametoa taarifa inayoelezea kuongezeka kwa hatari ya baa la njaa na milipuko ya magonjwa ya kuambukiza huku yakisisitiza muarobaini pekee kwa sasa ni kuruhusu njia mpya za kuingiza misaada ya kwenda kutatua changamoto zinazowakabili wananchi walioko Gaza. 

Sauti
3'34"