Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Watoto wakitembea kuelekea kituo cha wakimbizi wa ndani huko El Fasher, mji mkuu wa jimbo la Darfur Kaskazini nchini Sudan (Maktaba)
© UNICEF/Shehzad Noorani

Mfumo wa afya nchini Sudan unaporomoka: WHO

Nchini Sudan katika maeneo ambayo ni magumu kufikiwa, vituo vya afya vimeharibiwa, kuporwa au kukabiliwa na uhaba mkubwa wa wafanyakazi, madawa, chanjo, vifaa na vifaa. Ni asilimia 30 -20 tu ya vituo vya afya vinasalia kufanya kazi, na hata hivyo katika viwango vidogo, ameeleza leo Msemaji wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani, Christina Lindmeier.

Picha ya pamoja ya kikundi cha Washirika wa Maendeleo ya Kilimo na Lishe, wakulima, sekta binafsi, na watafiti na Taasisi za kitaaluma mjini Morogoro Tanzania.
UN News

FAO na wadau wawakutanisha wadau wa kilimo na chakula Tanzania

Nchini Tanzania, kwa ufadhili wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo (FAO) na wadau wake kama Kitovu cha Kuratibu Mifumo ya Chakula cha Umoja wa Mataifa, Kikundi cha Washirika wa Maendeleo ya Kilimo na Lishe, wakulima, sekta binafsi, na watafiti na Taasisi za kitaaluma wamekutana mjini Morogoro ili kupitia na kuboresha vipaumbele na ramani ya mifumo ya chakula iliyoanzishwa mwaka 2021.

Chumba cha Mahakama ya Kimataifa ya Haki ICJ, huko The Hague katika kesi ya Afrika Kusini dhidi ya sraeli.
© ICJ/Wendy van Bree

Gaza : ICJ imeitaka Israel kukomesha mashambulizi dhidi ya Rafah mara moja

Mahakama ya kimataifa ya haki ICJ leo imetoa maamuzi ya kesi ya Afrika Kusini dhidi ya Israel iliyowasilishwa Mei 10 ikiitaka ICJ kuiamuru Israel isitishe mara moja oparesheni zake zote za kijeshi na kuwezesha upatikanaji wa misaada ya kibinadamu. Na tarehe 16 na 17 Mei,kuhusu utekelezaji wa Mkataba wa Kuzuia na Kuadhibu Uhalifu wa Mauaji ya Kimbari katika Ukanda wa Gaza.

Sauti
1'54"