Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

UN News/George Musubao

MONUSCO tuko bega kwa bega na CENI DRC

Tayari Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, Félix Antoine Tshisekedi Tshilombo amethibitisha uchaguzi mkuu utafanyika nchini humo mwishoni mwa mwaka huu kama ilivyopangwa. Sasa ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, MONUSCO  unaeleza ni hatua gani zimefanyika na zinafanyika ili kuhakikisha uchaguzi huo unakuwa huru,a wahaki na unafanyika kwa amani.

Sauti
4'53"
Waziri wa mambo ya nje wa India, Subramaniam Jaishankar, akihutubia kikao cha 78 cha mjadala mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa.
UN Photo/Cia Pak

Katika enzi zilizoghubikwa na ubaguzi, mizozo na migawanyiko, diplomasia ndio suluhu pekee ya ufanisi: India

Waziri wa mambo ya nje wa India, Subramaniam Jaishankar, akihutubia kikao cha 78 cha mjadala mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa hii leo amesema kuwa katika wakati ambapo dunia inapitia misukosuko isiyo na kifani kuanzia mgawanyiko kati ya ulimwengu wa Mashariki na Magharibi unaoongezeka, na mvutano wa kimataifa baina ya Ulimwengu wa Kaskazini na Kusini kuzidi kuongezeka, diplomasia na mazungumzo ndio suluhisho pekee la ufanisi la kukabiliana na changamoto za sasa.

Siku ya Kimataifa ya Kutokomeza Silaha za Nyuklia huadhimishwa kila mwaka tarehe 26 Septemba.
© ICAN/Marlena Koenig

Tutaendelea kufuatilia mwenendo wa nyuklia Ukraine na kwingineko: IAEA

"Hatuendi popote, tutaendelea kufuatilia mwenendo wa nyuklia kila mahali", ni ujumbe kutoka kwa mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la nguvu ya nishati ya atomiki IAEA, Rafael Grossi, kuhusu dhamira ya shirika hilo kuendelea kufuatilia vinu vya nyuklia vya Ukraine wakati huu wa uvamizi unaoendelea wa Urusi lakini pia mwenendo wa nyuklia kwingineko duniani kama vile shughuli za uhakiki wa nyuklia nchini Iran na ufuatiliaji wa mipango ya nyuklia wa DPRK.