Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

MONUSCO tuko bega kwa bega na CENI DRC

Msemaji wa MONUSC, ofisi ya mjini Beni-Lubero Bwana Jean Tobie Okala

Tangu Januari 2023 MONUSCO imesafirisha maelfu ya tani za shehena nyeti sana za uchaguzi ambazo ni za CENI na zimewezesha shughuli za kurekodi na kuandikisha wapiga kura. -  Jean Tobie Okala, Msemaji MONUSCO Beni-Lubero.

UN News/George Musubao
Msemaji wa MONUSC, ofisi ya mjini Beni-Lubero Bwana Jean Tobie Okala

MONUSCO tuko bega kwa bega na CENI DRC

Haki za binadamu

Tayari Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, Félix Antoine Tshisekedi Tshilombo amethibitisha uchaguzi mkuu utafanyika nchini humo mwishoni mwa mwaka huu kama ilivyopangwa. Sasa ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, MONUSCO  unaeleza ni hatua gani zimefanyika na zinafanyika ili kuhakikisha uchaguzi huo unakuwa huru,a wahaki na unafanyika kwa amani.