Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Wanawake kutoka nchini Sudan wakitembea mahali salama Um Baru, Kaskazini mwa Darfur (Kutoka Maktaba).
UNAMID/Hamid Abdulsalam

ICC yaanzisha uchunguzi dhidi ya kuongezeka kwa ghasia Darfur Sudan

Mwendesha mashtaka wa Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu ICC amesema leo  kwamba anachunguza madai mapya ya uhalifu wa kivita na uhalifu dhidi ya binadamu katika jimbo la Darfur nchini Siudan, ikiwa ni pamoja na mauaji ya hivi karibuni ya watu 87 wa jamii ya kabila la Masalit, yaliyoripotiwa kutekelezwa na vikosi vya msaada wa haraka RSF Rapid na wanamgambo wake.

Shule ya Al-Imam Al-Kadhim kwenye mji wa Al-Geneina jimbo la Darfur Magharibi nchini Sudan, ambayo imekuwa hifadhi kwa wakimbizi wa ndani iliteketezwa kwa moto wakati huu ambapo mapigano yanaendelea nchini Sudan.
© Mohamed Khalil

OHCHR: Makaburi ya watu wengi yagunduliwa nchini Sudan

Miili ya takriban watu 87 ya kabila la Masalit na wengine wanaodaiwa kuuawa mwezi uliopita na vikosi vya msaada wa haraka RSF na washirika wao huko Darfur Magharibi nchini Sudan, imezikwa kwenye kaburi la pamoja huko El-Geneina kwa amri ya vikosi hivyo kulingana na taarifa za kuaminika ambazo Ofisi ya Haki za Kibinadamu ya Umoja wa Mataifa imezipata.