Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Muathirika wa ukatili wakingono mjini Goma DRC.
Picha ya UN/Marie Frechon (Maktaba)

Baraza la Usalama latakiwa kushughulikia uhalifu ‘ulionyamaziwa zaidi na unaokemewa kwa kiwango cha chini’

Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu kuhusu Unyanyasaji wa Kijinsia na Migogoro Pramila Patten, leo tarehe 14 Julai ameliambia Baraza la Usalama kwamba "ubakaji wa genge, utumwa wa kingono na aina nyingine za unyanyasaji wa kingono zinatumika kama mbinu ya vita, mateso na ugaidi kutisha na kufurusha watu.” 

Lawrence Oluwaseun Adeniyi raia wa Nigeria anayefanya shughuli zake Houston Marekani amewakilisha taasisi hii ya International Association of World Peace Advocates (IAWPA) katika Jukwaa la ngazi za juu kuhusu SDGs.
UN News

Amani ikitawala malengo ya maendeleo endelevu yatafanikishwa - Lawrence Oluwaseun Adeniyi

Jukwaa la ngazi ya juu la kisiasa kuhusu malengo ya maendeleo endelevu HLPF ambalo liling’oa nanga Julai 10, litafikia tamati tarehe 20 mwezi huu. Mmoja wa vijana walioshiriki katika mkutano hili ni Lawrence Oluwaseun Adeniyi, raia wa Nigeria anayefanya shughuli zake Houston Marekani ambaye amewakilisha taasisi hii ya International Association of World Peace Advocates (IAWPA) inayojitambulisha kwa kazi kuu mbili ambazo ni Utetezi wa Amani na Kuhakikisha Maendeleo Endelevu.

Sauti
2'45"
Mtoto akibeba maji kupitia eneo la kambi ya wakimbizi wa ndani ya Kanyaruchinya mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
© UNICEF/Arlette Bashizi

UNHCR imeonya dhidi ya kuongezeka kwa ukatili dhidi ya wanawake na wasicha Mashariki mwa DRC

Hali ya kusikitisha inajitokeza Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, ambapo ghasia zilizozuka upya kati ya makundi yasiyo ya kiserikali yenye silaha na vikosi vya serikali zimerejea katika majimbo ya Kivu Kaskazini, Kivu Kusini na Ituri zikiambatana na ukatili mkubwa dhidi ya wanawake na wasichana na kutawanya maelfu ya watu, limeonya leo shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR.

Sauti
2'41"