UN WOMEN kushirikiana na FIFA katika Kombe la Dunia la wanawake
Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na masuala ya wanawake UN WOMEN linashirikiana na Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani FIFA katika mashindano ya Kombe la Dunia la FIFA la wanawake yanayoanza tarehe 20 Julai mpaka 20 Agosti 2023 huko nchini Australia na New Zealand ambayo yanatarajiwa kutazamwa na zaidi ya watu bilioni mbili duniani kote, ikiwa ni hadhira kubwa zaidi katika historia ya mchezo mmoja wa wanawake.