Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Kathely Rosa, mwenye umri wa miaka 19 (kati awkiwa na mpira) akiwa na wahitimu wengine wa "One Win Leads to another", programu wa michezo nchini Brazil.
UN Women/Camille Miranda

UN WOMEN kushirikiana na FIFA katika Kombe la Dunia la wanawake

Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na masuala ya wanawake UN WOMEN linashirikiana na Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani FIFA katika mashindano ya Kombe la Dunia la FIFA la wanawake yanayoanza tarehe 20 Julai mpaka 20 Agosti 2023 huko nchini Australia na New Zealand ambayo yanatarajiwa kutazamwa na zaidi ya watu bilioni mbili duniani kote, ikiwa ni hadhira kubwa zaidi katika historia ya mchezo mmoja wa wanawake. 

Teknolojia ya droni nayo inaweza kuwa na manufaa bora au hasara kwa kutegemea inatumika kwenye misingi ipi. Hapa ni kwenye maonyesho ya ya mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu data uliofanyika Dubai 2018
IISD/ENB

Akili Mnemba (AI) ilete nuru na si giza – Katibu Mkuu UN

Hii leo Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limekuwa na mjadala wa wazi kuhusu amani na usalama duniani likimulika fursa na hatari zitokanazo na Akili Mnemba au Akili Bandia, AI ambapo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesihi Baraza hilo lioneshe uongozi katika nyanja hiyo hasa katika kuhakikisha teknolojia hiyo inatumika kujenga madaraja ya kijamii, kidijitali na kiuchumi badala ya kuleta utengano na uharibifu.

Mtoto akipokea chanjo ya polio nchini Burundi. (Maktaba)
© UNICEF Burundi

Hatua zimepigwa katika utoaji chanjo lakini changamoto bado zipo:WHO/UNICEF

Takwimu mpya zilizotolewa leo na mashirika ya Umoja wa Mataifa lile la afya duniani WHO na la kuhudumia watoto UNICEF, zinaonyesha dalili za huduma za chanjo kuongezeka katika baadhi ya nchi, lakini bado huduma hizo hazifikii viwango vya kabla ya janga la COVID-19, hasa katika nchi zenye kipato cha chini, na hivyo kuwaweka watoto katika hatari kubwa ya kupata maambukizi na milipuko ya magonjwa.