Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Katibu Mkuu wa UN António Guterres alipokutana na familia ya wakimbizi wa ndani katika kambi ya Baidoa kusini magharibi mwa Somalia.
UN Photo/Sourav Sarker

Akiwa katika ziara ya kushitukiza Guterres aichagiza jumuiya ya kimataifa kuishika mkono Somalia

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres akiendeleza utamaduni wa mshikamano na mataifa ya Kiislam  wakati wa mwezi mtukufu wa mfungo wa Ramadhan leo amewasili Somalia ambako amesisitiza haja ya jumuiya ya kimataifa kuishika mtono nchi hiyo ya Pembe ya Afrika na kuipunguzia madhila ya kibinadamu na kusaidia juhudi za serikali za kujijenga upya.

Wadau wa afya serikalini na wafadhili kwenye kongamano la kwanza la taifa la saratani nchini Kenya.
UN News Nairobi/Thelma Mwadzaya

Saratani ikigundulika mapema inatibika na kupona hivyo upimaji ni muhimu sana: WHO

Saratani ni muiongoni mwa magonjwa yasiyo ya kuambyukiza ambayo tyanakatili Maisha ya mamilioni ya watu kila mwaka, ndio maana shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO na wadau wengine wa kupambana na saratani wanapigia upatu upimaji wakiamini kwamba siku zote kinga ni bora kuliko kuponya, kwani saratani ikigundulika mapema inatibika na mgonjwa kupona.

Wakati wa siku ya afya duniani 7 Aprili 2023, walinda amani wa UN kutoka kikosi cha Tanzania cha kutoa msaada wa haraka, TANZQRF katika kwneye ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani, MONUSCO nchini DRC  wametoa huduma za kupima magonjwa yasiyo ya ku…
TANZQRF3/Methew Makoba

Siku ya Afya Duniani: Walinda amani wa UN kutoka TZ nchini DRC waadhimisha kwa vitendo

Leo ni siku ya afya duniani ujumbe ukiwa ni Afya kwa Wote ambapo walinda amani wa Umoja wa Mataifa kutoka Tanzania wanaohudumu kwenye ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, DRC, MONUSCO, wametumia siku hii kuwapima magonjwa yasiyo ya kuambukiza, NCDs, wakazi wa Beni-Mavivi jimboni Kivu.

Sauti
4'41"
Kikosi cha Walinda Amani wa Tanzania, TANBAT 6 wanaohudumu chini ya ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati – MINUSCA wakitoa huduma ya maji safi na salama kwa jamii mjini Berberati mkoa wa Mambéré-Kadéï.
TANBAT6/Kapteni Mwijage

TANZBAT6 watoa huduma ya maji kwa wananchi nchini CAR

Kikosi cha sita cha walinda amani wa Umoja wa Mataifa kutoka Tanzania wanaohudumu chini ya ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati – MINUSCA wametoa huduma ya maji safi na salama kwa vijiji vinavyokabiliwa na uhaba wa maji mjini Berberati mkoa wa Mambéré-Kadéï. 

Sauti
2'27"
Mvulana akiwa amesimama kwenye daraja juu ya mto Sanate huko Higuey, moja ya maeneo yaliyoathiriwa zaidi na kimbunga Fiona huko Jamhuri ya Dominika, Amerika ya Kati.
© UNICEF/Ricardo Rojas

Vimbunga: Asili ya majina hadi kuondolewa kwenye orodha

Hivi karibuni shirika la Umoja wa Mataifa la Hali ya Hewa duniani, WMO  kupitia kamati yake inayosimamia masuala ya vimbunga liliondoa katika orodha ya vimbunga ya kitropiki kwenye bahari ya Atlantiki majina Fiona na Ian. WMO kupitia taarifa yake hiyo iliweka bayana sababu za uamuzi huo kuwa ni madhara makubwa yaliyosababisha vimbunga hivyo huko Amerika ya Kati, Karibea, Marekani na Canada