Mshikamano, uongozi na kujitolea kunahitajika ili kufikia malengo ya maendeleo ya 2030: Mohammed
Ingawa mizozo ya kimataifa inayoendelea inadhoofisha mafanikio ya maendeleo yanayopiganiwa kwa bidii, "sasa si wakati wa kukata tamaa", Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Amina Mohammed amewaambia mawaziri wa Afrika na watunga sera waliokutana mjini Niamey, Niger, hii leo.