Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Watoto wakimbizi kutoka Somalia wakiwa kwenye kambi ya wakimbizi ya Daadab nchini Kenya ambako WFP inawapatia misaada ya dharura.
WFP/Rose Ogola

Majanga yanavyozidi kushamiri isiwe kisingizio cha kusigina haki za mtoto- UN

Wataalamu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa hususan zile za mtoto wametoa taarifa ya pamoja hii leo huko Geneva, Uswisi wakisema  majanga ya kiafya, kibinadamu na yale  yanayohusiana na tabianchi yakizidi kuongeza changamoto kubwa duniani kila uchao kama vile ukimbizi wa ndani, ukatili wa kingono na njaa, serikali lazima zikumbuke kuwa watoto wana haki kamilifu za kimsingi za kibinadamu na kwamba haki hizo zinapaswa kulindwa.

Isha Dyfan akizungumza na wanahabari mwishoni mwa ziara yake SOmalia mapema mwaka huu.
UN Photo / Fardosa Hussein

Haki ya Uhuru wa kujieleza Somalia mashakani, wanahabari na watetezi wa haki matatani- Ripoti

Isha Dyfan, Mtaalam Huru wa hali ya haki za binadamu nchini Somalia, hii leo jijini Geneva, Usiwisi akiwasilisha ripoti ya hali ya haki za binadamu nchini Somalia, amelieleza Baraza la Haki za Binadamu  la Umoja wa Mataifa kuwa ripoti za matukio ya ukiukwaji wa haki za binadamu dhidi ya waandishi wa habari na watetezi wa haki za binadamu nchini Somalia zinatia wasiwasi mkubwa.