Mradi wa ILO waleta matumaini kwa watamil nchini Sri Lanka
Nchini Sri Lanka, serikali na mradi wa pamoja wa Umoja wa Mataifa kwa ajili ya amani kupitia shirika la Umoja wa Mataifa la kazi duniani, ILO, wanatekeleza mradi wa kuinua jamii za watamil ambazo zimerejea kwenye makazi yao baada ya mzozo wa muda mrefu kaskazini mwa nchi hiyo, mradi ambao unawezesha jamii kujumuika tena na kushiriki kwenye shughuli za kiuchumi na kuinua kipato chao baada ya mzozo uliodumu kwa takribani miaka 25.