Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Akina mama wakisubiri na watoto wao ili wapatiwe chanjo kupitia mradi unaosaidiwa na UNFPA
UNFPA/Ralph Tedy Erol

Haiti hali si shwari, viwango vya juu zaidi vya njaa vyaripotiwa kwa mara ya kwanza

Msururu wa majanga yasiyo na huruma yanazidi kukumba wananchi wa Haiti kila uchao na kusababisha taifa hilo kuwa katika mkwamo,yameonya mashirika mawili ya Umoja wa Mataifa lile la chakula na kilimo duniani, FAO na la mpango wa chakula duniani, WFP kupitia taarifa yao waliyoitoa leo hii kutoka mji mkuu wa Haiti, Port- au- Prince. Mashirika hayo yanasema nusu ya wananchi wa Haiti wanakabiliwa na uhaba mkubwa zaidi wa chakula.

Baadhi ya matatizo ya ugonjwa wa kisukari ni upofu,kiharusi na kuharu figo.Roseane wa Brazil ana aina ya pili ya Kisukari.
WHO/Eduardo Martino

Watu bilioni 2.2 wana uoni hafifu au upofu duniani kote:WHO 

Shirika la afya duniani WHO limetoa rai ya kuhakikisha fursa ya huduma za macho zilizo bora, jumuishi na kwa wote zinapatikana wakati huu ambapo takriban watu bilioni 2.2 kote duniani wanaishi na changamoto ya uoni hafifu au upofu. Taarifa zaidi inasomwa na Happiness Pallangyo wa Radio washirika Uhai FM. 

Sauti
2'39"
Vifaa vya kuchezea na kujifunzia watoto vilivyotengenezwa na watumishi wa kujitolea nchini Zambia kwa ajili ya kutumiwa na watoto kwenye vituo vya maendeleo ya mapema ya mtoto, ECD vinavyoendeshwa na UNICEF Zambia.
© UNICEF/Kinny Siakachoma

Mradi wa kusoma na kuhesabu waleta manufaa kwa wanafunzi nchini Zambia

Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulika na masuala ya watoto UNICEF nchini Zambia kwa kushirikiana na serikali ya Zambia na Taasisi ya Hampel wanaendesha programu iitwayo Catch Up yenye lengo la kuwasaidia wanafunzi wa shule za msingi nchini humo kupata matokeo bora ya masomo ya hisabati na kusoma hususan wale waliokuwa na ufaulu mdogo wa masomo hayo na sasa matokeo chanja yameanza kuonekana.

Watu milioni mbili na nusu nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati ( CAR)wanakabiliwa na njaa
WFP/Bruno Djoye

Hatua zichukuliwe sasa ama mamilioni zaidi watatumbukia kwenye njaa:WFP

Dunia ipo hatarini kuingia katika mwaka mwingine wenye uhaba wa chakula wakati huu ambapo watu wengi tayari wanazidi kuingia katika dimbwi la  uhaba wa chakula, limeonya shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula duniani WFP ambalo limetoa wito wa hatua za haraka kuchukuliwa kushughulikia mzizi wa tatizo hili wakati dunia ikielekea kuadhimisha siku ya chakula duniani hapo Oktoba 16.

 Wakimbizi wa Sudan kutoka jimbo la Blue Nile, wanaoishi katika kambi ya Doro katika jimbo la Upper Nile nchini Sudan Kusini
Photo UNHCR/V. Tan

Asanteni watu wa White Nile kuwapokea wakimbizi wa ndani kutoka Blue Nile - Khardiata Lo N’Diaye

Mratibu wa Masuala ya Kibinadamu nchini Sudan, Khardiata Lo N’Diaye hii leo akizungumzia kuhusu kuhamishwa kwa wakimbizi wa ndani (IDPs) kuelekea Jimbo la White Nile ametoa shukrani kwa serikali ya Jimbo la White Nile na “muhimu zaidi, jumuiya za Kosti na Rabak. Wametoa makazi na usaidizi unaohitajika kwa watu hawa waliofurushwa, zaidi ya watu 19,000 kati yao waliishi katika White Nile.”