Viongozi wa Afrika wazindua mpango wa ‘Eduation Plus’ kusaidia wasichana kuendelea na shule
Viongozi waliokutana katika mkutano wa Muungano wa Afrika mjini Lusaka, Zambia hii leo wameahidi kuunga mkono mpango wa ‘Education Plus’ wakijitolea kuchukua hatua ya kuwafanya wasichana kubaki shuleni, jambo ambalo litapunguza kwa kiasi kikubwa uwezekano wao wa kuambukizwa Virusi Vya UKIMWI, VVU.