Tanzania, ILO, na wadau wanusuru watoto kutumikishwa kwenye mashamba ya tumbaku
Tanzania imeridhia mikataba yote muhimu ya kimataifa ya kuzuia ajira kwa watoto na imeendelea kutekeleza mipango ya kuwaondoa watoto katika mazingira magumu kama hayo. Kwa msaada wa wadau mbalimbali - kama vile Umoja wa Mataifa kupitia shirika lake la kazi duniani, ILO, mashirika yasiyo ya kiserikali na mashirika ya kiraia - sheria na sera zilizopo zimebadilishwa ili kutoa haki bora na ustawi.