Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Wakulima wakitayarisha tumbaku tayari kuuza soko ya Mzingo, Malawi.
© FAO/Amos Gumulira

Tanzania, ILO, na wadau wanusuru watoto kutumikishwa kwenye mashamba ya tumbaku

Tanzania imeridhia mikataba yote muhimu ya kimataifa ya kuzuia ajira kwa watoto na imeendelea kutekeleza mipango ya kuwaondoa watoto katika mazingira magumu kama hayo. Kwa msaada wa wadau mbalimbali - kama vile Umoja wa Mataifa kupitia shirika lake la kazi duniani, ILO, mashirika yasiyo ya kiserikali na mashirika ya kiraia - sheria na sera zilizopo zimebadilishwa ili kutoa haki bora na ustawi.

Emma Theofelus ambaye ni Naibu Waziri wa Habari wa sasa nchini Namibia na mshindi wa tuzo ya UNFPA.
UNFPA

Emma Theofelus wa Namibia na BKKBN ya Indonesia ndio washindi wa Tuzo ya UNFPA mwaka 2022 

Tuzo ya kila mwaka ya shirika la Umoja wa Mataifa la idadi ya watu na afya ya uzazi, UNFPA ambayo hutolewa kwa mtu binafsi na shirika au taasisi inayojikita katika kuboresha afya ya uzazi kwa wanawake, pamoja na afya ya akina mama na wajawazito, mwaka huu imeenda kwa Emma Theofelus ambaye ni Naibu Waziri wa Habari wa sasa nchini Namibia na mshindi wa kwanza mwenye umri mdogo zaidi kuwahi kupata tuzo hiyo.

Sauti
3'12"
Lucas na kaka yake wote wana  ualbino ambao unasababisha ngozi yao kupata matatizo na uoni wao ni hafifu.
UNICEF

Tuwajumuishe watu wenye ualbino kwenye mijadala:UN 

Ikiwa leo dunia inaadhimisha siku ya kimataifa ya kuelimisha jamii kuhusu watu wenye ualbino, Umoja wa Mataifa umetoa  rai kwa nchi zote duniani kuwajumuisha watu wenye ualbino katika mijadala na mipango inayoathiri haki zao za kibinadamu, ili kuhakikisha wanafurahia usawa na ulinzi unaotolewa kwao katika sheria na viwango vya kimataifa.

Audio Duration
2'24"
Wakati wa uhamasishaji dhidi ya utumikishaji watoto kwenye vikundi vilivyojihami huko Kalemie, ikiwa ni harakati za ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, MONUSCO.
MONUSCO \ Marcelline Comlan

Afrika yaongoza duniani kwa utumikishaji watoto

Leo tarehe 12 Juni, kama ilivyo ada ya kila mwaka, jumuiya ya kimataifa inaungana na kusema hapana kwa ajira ya watoto. Licha ya kupungua kwa idadi ya watoto wanaofanya kazi katika miongo miwili iliyopita, maendeleo kuelekeza kutokomeza ajira kwa watoto yalitatizwa katika kipindi cha mwaka 2016 hadi 2020.