Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Madarasa yako wazi lakini elimu inaendelezwa kwa kutumia teknolojia wakati huu wa kukabiliana na COVID-19
CC0 Public Domain

Elimu ya watu wazima, 'ngumbaru' haiwafikii wenye uhitaji zaidi - UNESCO 

Changamoto kuu ya kujifunza na elimu ya watu wazima kote ulimwenguni ni kufikia wenye uhitaji zaidi. Huo ndio ujumbe muhimu wa Ripoti ya Tano ya kimataifa ya shirika la Umoja wa Mataifa la elimu, Sayansi na Utamaduni, UNESCO kuhusu Mafunzo na Elimu ya Watu Wazima (GRALE 5) ambayo imewekwa wazi leo tarehe 15 Juni 2022 katika Mkutano wa Saba wa Kimataifa wa Elimu ya Watu Wazima huko Marrakech, Morocco. 

Mwanamke mzee akiwa katika kambi ya wakimbizi wandani nchini Somalia
© UNICEF/Sebastian Rich

WHO yatoa vipaumbele 5 kukabiliana na unyanyasaji wa wazee

Leo ni siku ya kuhamasisha kupinga unyanyasaji dhidi ya wazee na katika kuadhimisha siku hii Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ulimwenguni WHO na wadau wake wamechapisha vipaumbele vitano vitakavyosaidia kuzuia na kukabiliana na unyanyasaji wa wazee na hivyo kuchangia katika kuboresha afya, utawi na utu wao.

Mji wa Bucha umeharibiwa vibaya kufuatia mashambulio Kyiv, mji mkuu wa Ukraine.
© WFP/Marco Frattini

Taarifa za awali zadokeza uhalifu wa kivita na ukiukwaji wa haki za binadamu Ukraine- Kamisheni 

Kamisheni iliyoundwa na Baraza la Umoja wa Mataifa la Haki za Binadamu kuchunguza madai ya ukiukwaji wa haki za binadamu na sheria za kimataifa za kibinadamu nchini Ukraine imetoa ripoti ya ziara yake ya kwanza nchini Ukraine na kusema ingawa haiko katika nafasi ya kuwa na vigezo vya kisheria au matokeo kamilifu, taarifa za awali zinadokeza kuweko kwa ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu na sheria za kimataifa za kiutu. 

Muuguzi akimpa mama chanjo dhidi ya Covid 19
© UNICEF/Zahara Abdul

WHO latoa mwongozo wa chanjo ya Monkeypox

Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ulimwenguni WHO limetoa taarifa ya kupungua kwa asilimia 90 kwa vifo vitokanavyo na ugonjwa wa COVID-19, mwongozo wa chanjo dhidi ya ugonjwa wa Monkeypox na kueleza suala la utapiamlo katika pembe ya Afrika likisema umefika katika ngazi ya 3 ikiwa ni ngazi ya juu zaidi katika viwango vya shirika hilo.