Elimu ya watu wazima, 'ngumbaru' haiwafikii wenye uhitaji zaidi - UNESCO
Changamoto kuu ya kujifunza na elimu ya watu wazima kote ulimwenguni ni kufikia wenye uhitaji zaidi. Huo ndio ujumbe muhimu wa Ripoti ya Tano ya kimataifa ya shirika la Umoja wa Mataifa la elimu, Sayansi na Utamaduni, UNESCO kuhusu Mafunzo na Elimu ya Watu Wazima (GRALE 5) ambayo imewekwa wazi leo tarehe 15 Juni 2022 katika Mkutano wa Saba wa Kimataifa wa Elimu ya Watu Wazima huko Marrakech, Morocco.