Shida na changamoto nyingi zinazowakumba wanawake ni kutokana na mfumo dume na uchu wa madaraka: Guterres

Mwakilishi mwanamke akichagiza wanawake wengine kupaza sauti zao Rajasthan, India.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema pamoja na kuwepo kwa maazimio na sheria nyingi za kuhimiza usawa kwenye jamii, wanawake na wasichana kila kona ya dunia wanaendelea kuteseka, kunyanyasika na kuonewa na yote haya ni kutokana na kuwepo kwa mizizi ya mfumo dume na uchu wa madaraka.