Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Watoto wa Darfur Kaskazini kambi ya wakimbizi wa ndani ya Abo Shouk ambako UNAMID imekarabati darasa.
UN Photo/Albert Gonzalez Farran

Vita, Machafuko na majanga mengine vyatawanya watoto milioni 36.5 mwaka 2021: UNICEF 

Vita, machafuko na mjanga mengine vimewaacha watoto milioni 36.5 wakitawanywa kutoka majumbani kwao hadi kufikia mwisho wa mwaka 2021 kwa mujibu wa takwimu mpya zilizotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF ambalo linasema idadi hiyo ni kubwa kabisa kurekodiwa tangu vita ya pili ya dunia.

Sauti
3'36"
Wafanyakazi wa majumbani hawana uhifadhi wa jamii
UN Women/Joe Saad

Asilimia 6 tu ya wafanyakazi wa majumbani duniani ndio wenye ulinzi wa hifadhi ya jamii:ILO 

Katika siku ya kimataifa ya wafanyakazi wa majumbani ripoti mpya iliyotolewa leo na shirika la kazi duniani imesema ni asilimia 6 pekee ya wafanyakazi hao ndio wenye ulinzi wa hifadhi ya jamii na hivyo kuwaacha asilimia 94 ya wafanyakazi hao kote duniani wakikosa fursa ya ulinzi muhimu wa kijamii unaojumuisha matibabu, magonjwa, ukosefu wa ajira, uzee, ajali kazini, familia, malipo ya uzazi, ulemavu na marupurupu mengine.