Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Bi. Joyce Msuya, Msaidizi wa Katibu Mkuu wa UN na Naibu Mkuu wa Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kuratibu misaada ya dharura, OCHA katika mahojiano na UN News Kiswahili Aprili 2022 New York, Marekani.
UN/ Anold Kayanda

Ukame Pembe ya Afrika: UN katu haiwezi kusahau licha ya majanga mengine duniani

Licha ya majanga mengine ya kibinadamu yanayoendelea duniani ikiwemo kule Ukraine, bado Umoja wa Mataifa unahangaika kila uchao kuhakikisha inasaidia wakazi wa Pembe ya Afrika ambako ukame umesababisha watu milioni 15 kukosa uhakika wa chakula, amesema Joyce Msuya Msaidizi wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa na Naibu Mkuu wa ofisi ya Umoja wa Mataifa inayoratibu misaada ya dharura, OCHA.

 

Moja ya mitaa ya mji mkuu wa Rwanda, Kigali
UN/Rick Bajornas

Tunazifuatilia taarifa kuwa Uingereza inataka kuwahamishia nchini Rwanda wasaka hifadhi  

Kufuatia uwepo wa taarifa za kuwa Uingereza imeingia makubaliano na Rwanda ya kuwahamisha wasaka hifadhi nchini Uingereza na kuwapeleka Rwanda, Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR limesema linaelewa kuwa serikali ya Uingereza inatangaza ushirikiano wa uhamiaji na maendeleo ya kiuchumi na nchi ya Rwanda lakini linahitaji kuyaona makubaliano hayo kwanza kabla ya kutoa maoni.

Sauti
1'21"