UNICEF yahakikisha watoto DRC wanasoma licha ya changamoto
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF linajitahidi kwa kadri ya uwezo wake kuhakiisha watoto walioko kwenye kituo cha makazi ya muda cha Rhoe kwenye jimbo la Ituri nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC wanaendelea kupata haki yao ya msingi ya elimu licha ya mazingira wanamoishi.