Mlipuko mpya wa Ebola wazuka Mbandaka DRC:WHO
Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC leo imetangaza mlipuko mpya wa Ebola katika jimbo la kaskazini-magharibi baada ya kisa kuthibitishwa huko Mbandaka, jiji lililo katika jimbo la Equateur.
Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC leo imetangaza mlipuko mpya wa Ebola katika jimbo la kaskazini-magharibi baada ya kisa kuthibitishwa huko Mbandaka, jiji lililo katika jimbo la Equateur.
Kama iliyo kwa wavulana wengi duniani, Aweys Haji Nur kutoka Somalia alipokuwa mdogo alikuwa na ndoto ya kuwa mwanasoka wa kulipwa.
Hatimaye filamu ya Tanzania The Royal tour iliyotengenezwa kuonesha vivutio vya utalii katika taifa hilo la Afrika Mashariki imezinduliwa nchini Marekani huku Msemaji Mkuu serikali ya Tanzania akisema filamu hiyo itakuwa mkombozi wakati huu ambapo mataifa mbalimbali ikiwemo Tanzania zinahaha kujikwamua kiuchumi baada ya janga la ugonjwa wa Corona au COVID-19.
Uvamizi wa Urusi karibu miezi miwili iliyopita umeitumbukiza Ukraine katika mzozo wa haki za binadamu na janga la kibinadamu ambalo limeharibu maisha ya raia kote nchini na kwingineko, amesema leo kamishna mkuu wa Umoja wa Mataifa wa Haki za Kibinadamu Michelle Bachelet huku akizitaka pande zote husika katika mzozo huo kuheshimu sheria za kimataifa za haki za binadamu na hasa kanuni zinazosimamia masuala ya uhasama.
Katika kuadhimisha siku ya kimataifa ya Mama Sayari dunia hii leo, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametaka kufanyika kwa kila liwezekanalo kumlinda mama huyo kwa kuwa yuko mmoja tu na hakuna mbadala.
Katika kipindi cha miezi miwili iliyopita, Ukraine imeshuhudia "mateso, madhila na uharibifu kwa kiwango kikubwa", amesema mratibu wa Umoja wa Mataifa kuhusu mgogoro wa Ukraine akizungumza na waandishi wa habari hii leo mjini Lviv Msagharibi mwa Ukraine, na kumuunga mkono Katibu Mkuu kwa kusema, "lazima tukomeshe umwagaji damu na Uharibifu nchini humo".
Zaidi ya watoto milioni 1 nchini Ghana, Kenya na Malawi sasa wamepokea dozi moja au zaidi ya chanjo ya kwanza ya malaria duniani, kutokana na mpango wa majaribio ulioratibiwa na shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO.
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR, limeeleza kushtushwa kwake na ripoti ya vifo vya wasaka hifadhi 6 vilivyotokea wakati wakijaribu kutoroka kutoka kituo cha muda cha uhamiaji kwenye jimbo la Penang, kaskazini mwa Malaysia.
Nchini Kenya harakati za shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF za kuondoa fikra potofu katika kaunti ya Kisumu kuhusu chanjo dhidi ya Corona au COVID-19 zimezaa matunda na sasa hata wale waliokuwa wamesita kupata chanjo hiyo wameanza kupata.
Kutana na Agnes mkulima kutoka wilaya ya Lodwar kaunti ya Turkana jimbo la Rift Valley nchini Kenya. Mabadiliko ya tabianchi yanayolikumba eneo la Afrika Mashariki kwa kiasi kikubwa yamemuathiri sana yeye na jamii yake, lakini sasa asante kwa mradi wa pamoja wa mashirika ya Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani WFP na la chakula na kilimo FAO wa kuwasaidia wakulima wadogo kujenga mfereji wa maji kwa ajili ya umwagiliaji na kununua mazao yao, maisha ya Agnes na jamii yake yamebadilika.