Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

UNICEF yawasaidia waliokumbwa na mafuriko Namibia

Shirika la umoja wa mataifa linalohusika na watoto UNICEF limeendelea na operesheni yake ya utoaji wa huduma za dharura katika eneo la Kaskazini mwa Namibia ambako mamia ya watu wako kwenye hali mbaya kufuatia mvua kubwa iliyosababisha mafuriko yasiyopata kushuhudiwa kwa miaka 120 iliyopita.

Pillay akamilisha ziara yake nchini Mauritania

Mkuu wa shirika la haki za binadamu la Umoja wa Mataifa Navi Pillay amekamilisha ziara ya siku mbili nchini Mauritania ambapo alizungumzia changamoto za masuala ya haki binadamu zinazoikabili nchi hiyo na maafisa wa ngazi za juu serikalini pamoja na waakilishi wa mashirika ya umma.