Srgjan Kerim ana matumaini mema juu ya mageuzi katika BU
Raisi aliyepita wa kikao cha 62 cha Baraza Kuu, Srgjan Kerim, ambaye alimaliza muda wake Ijumatatu, (15/09/08) alipokutana na waandishi habari wa kimataifa waliopo Makao Makuu hapo jana, alibainisha ya kuwa kulipatikana mafanikio makubwa kwenye kazi za Baraza, chini ya uongozi wake, hasa pale wajumbe wa kimataifa waliporidhia kuzingatia uwezekano wa kurekibisha na kuleta mageuzi kwenye mfumo wa Baraza la Usalama.