Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Srgjan Kerim ana matumaini mema juu ya mageuzi katika BU

Raisi aliyepita wa kikao cha 62 cha Baraza Kuu, Srgjan Kerim, ambaye alimaliza muda wake Ijumatatu, (15/09/08) alipokutana na waandishi habari wa kimataifa waliopo Makao Makuu hapo jana, alibainisha ya kuwa kulipatikana mafanikio makubwa kwenye kazi za Baraza, chini ya uongozi wake, hasa pale wajumbe wa kimataifa waliporidhia kuzingatia uwezekano wa kurekibisha na kuleta mageuzi kwenye mfumo wa Baraza la Usalama.

Nchi 17 zakubali mapendekezo ya kudhibiti kisheria vitendo vya makampuni ya wanajeshi wa kukodi

Wataalamu kutoka nchi 17 waliokutana kwenye kikao maalumu kwenye mji wa Montreux, Uswiss kuanzia Ijumatatu (15/09/08), kuzingatia udhibiti bora wa shughuli za yale makampuni ya wanajeshi wa binafsi wanaohudumia usalama, hii leo wamepitisha warka maalumu uliosisitiza ya kuwa Serikali za Mataifa zina dhamana kuu ya kuhakikisha askari wakandarasi wa binafsi wanaokodiwa kushiriki kwenye maeneo ya uhasama na vita huwa wanafuata sheria za kiutu za kimataifa.

Hapa na Pale

Baraza la Usalama lilikutana asubuhi, kwenye kikao cha faragha, kushauriana juu ya masuala ya usalama na amani katika bara la Afrika. Kwenye mashauriano ya asubuhi Baraza lizingatia taarifa kuhusu mzozo wa karibuni kati ya Eritrea na Djibouti, ripoti ambayo iliwakilishwa mbele ya wajumbe wa Baraza hilo na Joaõ Honwana, Mkurugenzi wa Kitengo cha Afrika katika Idara ya UM juu ya Masuala ya Kisiasa (DPA). Kadhalika, Baraza liliilia “mada nyenginezo” ambazo hatujadhihirishiwa hasa zinahusika na nini.

Haki za Binadamu zinazorota Sudan, adai Sima Samar

Baraza la Haki za Binadamu Geneva leo limezingatia ripoti iliowasilishwa na Sima Samar, Mkariri Maalumu juu ya hali ya haki za binadamu katika Sudan. Alisema alipowasilisha ripoti, ya kwamba hali nchini humo bado inakabiliwa na vizingiti kadha wa kadha vyenye kutatanisha utekelezaji unaofaa wa haki za binadamu Sudan.

ICRC inasema Usomali inahitajia misaada ya kihali

Marcel Izard, Msemaji wa Kamati ya Kimataifa ya Msalaba Mwekundu na Hilali Nyekundu (ICRC) aliwaambia waandishi habari leo Geneva kwamba hali katika Usomali bado inaendelea kuharibika na shirika lao linajaribu kuhudumia umma muathiriwa mahitaji yao ya kimsingi.~

Kikao cha 62 cha Baraza Kuu kimekamilisha shughuli zake

Ijumatatu usiku kikao cha 62 cha Baraza Kuu la UM kilikamilisha shughuli zake kwa kupitisha maazimio kadha. Moja ya azimio muhimu liliopitishwa mkutanoni, kwa kauli moja, ni lile pendekezo la kuanzisha tena, kabla ya tarehe 28 Februari mwakani, majadiliano ya kupanua uwanachama wa Baraza la Usalama. Azimio hili lilipitishwa baada ya mivutano ya saa nyingi kati ya wawakilishi wa kutoka Mataifa Wanachama.~

Hapa na Pale

Mashirika ya UM ya UNICEF, WHO na washiriki wanaohudumia misaada ya kiutu yamejumuika nchini Zimbabwe kukabili maradhi ya kipindupindu yalioripotiwa kuzuka katika vitongoji vya mji mkuu wa Harare, ambapo inaripotiwa watu 11 walifariki na 80 wengine waliambukizwa na maradhi hayo. UNICEF ikishirikiana kwa ukaribu zaidi na wenye madaraka wenyeji, pamoja na mashirika yasio ya kiserikali na WHO, imenzisha vituo viwili vya matibabu kuwasaidia wagonjwa wa kipindupindu. Zahanati hizo zinaendeshwa na lile shirika la madaktari wa kimataifa lijulikanalo kama Médecins Sans Frontières.