Kikao cha 62 cha Baraza Kuu kimekamilisha shughuli zake
Ijumatatu usiku kikao cha 62 cha Baraza Kuu la UM kilikamilisha shughuli zake kwa kupitisha maazimio kadha. Moja ya azimio muhimu liliopitishwa mkutanoni, kwa kauli moja, ni lile pendekezo la kuanzisha tena, kabla ya tarehe 28 Februari mwakani, majadiliano ya kupanua uwanachama wa Baraza la Usalama. Azimio hili lilipitishwa baada ya mivutano ya saa nyingi kati ya wawakilishi wa kutoka Mataifa Wanachama.~