Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Hapa na Pale

Hapa na Pale

Baraza la Usalama lilikutana asubuhi, kwenye kikao cha faragha, kushauriana juu ya masuala ya usalama na amani katika bara la Afrika. Kwenye mashauriano ya asubuhi Baraza lizingatia taarifa kuhusu mzozo wa karibuni kati ya Eritrea na Djibouti, ripoti ambayo iliwakilishwa mbele ya wajumbe wa Baraza hilo na Joaõ Honwana, Mkurugenzi wa Kitengo cha Afrika katika Idara ya UM juu ya Masuala ya Kisiasa (DPA). Kadhalika, Baraza liliilia “mada nyenginezo” ambazo hatujadhihirishiwa hasa zinahusika na nini.