Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Kikao cha 63 cha Baraza Kuu la UM chafunguliwa rasmi

Majadiliano ya jumla ya Baraza Kuu la UM, kwenye kikao cha wawakilishi wote yalianzishwa rasmi asubuhi ya leo ambapo viongozi wa kimataifa waliwasilisha hoja zao kadha wa kadha kuhusu utaratibu unaofaa kuzingatiwa kimataifa ili kukabiliana na matatizo ya ulimwengu kipamoja.

Rais wa Baraza Kuu ahimiza ushikamanao kukabili matatizo ya ulimwengu

Rais wa Baraza Kuu la UM, Miguel d’Escoto Brockmann alipofungua majadiliano ya jumla ya kikao cha mwaka huu cha 63 cha UM, aliwaambia wawakilishi wa Mataifa Wanachama 192 ya kwamba wakati umewadia kwa umma wa kimataifa “kuchagua njia iliyoongoka ya ushikamano na umoja” kukomesha kile alichokiita utamaduni wa uchoyo na ubinafsi, ustaarabu, ambao alisihi husababisha mamilioni ya umma wa ulimwengu kusumbuliwa na umaskini pamoja na matatizo mengineyo yalizushwa na wanadamu wenyewe.

Hapa na pale (Taarifa za kusoma)

Kikao cha 63 Baraza Kuu la UM kiliongozwa na Raisi wa mwaka huu Miguel d’Escoto Brockmann wa Nicaragua. Kabla ya Raisi wa Baraza Kuu kufungua rasmi majadiliano ya wawakilishi wote, KM wa UM Ban Ki-moon alihutubia kikao kwenye ukumbi wa Baraza Kuu ambapo aliwasilisha taarifa ya mapitio ya mwaka kuhusu shughuli za UM ulimwenguni. Baada ya hapo Raisi Miguel d’Escoto alihutubia wawakilishi wa Mataifa Wanachama 192, na alifuatiwa na Raisi Luiz Inácio Lula da Silva wa Brazil ambaye taifa lake, kwa kulingana na mila za UM, huwa ni taifa la awali kuongoza majadiliano ya jumla kwenye Baraza Kuu.

Viongozi wa dunia watathminia maendeleo Afrika

Baraza Kuu la UM leo hii limeanzisha mkutano maalumu wa watu wa ngazi za juu, kuzingatia, kwa sikui nzima, mahitaji ya maendeleo kwa bara la Afrika, kwa sababu ya wasiwasi uliojiri wenye kuonyesha bara la Afrika lipo nyuma sana, tukilinganisha na maeneo mengine, katika kutekeleza ile kampeni ya kimataifa ya kupunguza kwa nusu, katika 2015, hali ya ufukara, kutojua kusoma na kuandika na maradhi mengineyo ya kijamii.

WFP inaomba msaada wa kuhudumia chakula mamilioni Ethiopia

Shirika la UM juu ya Miradi ya Chakula Duniani (WFP) limetangaza ilani maalumu ya maombi ya kufadhiliwa dola milioni 460 kuhudumia chakula watu milioni 9.6 katika Ethiopia ambao wameathirika vibaya sana kutokana na ukame uliotanda kwenye maeneo yao ikichanganyika na mifumko hatari ya bei za chakula.

Mwendesha Mashtaka wa ICC awasiliana na viongozi wa kimataifa juu ya Darfur

Luis Moreno Ocampo, Mwendesha Mashtaka wa Mahakama ya Kimataifa juu ya Makosa ya Jinai ya Halaiki (ICC) yupo New York kwa madhumuni ya kuwasiliana na watendaji wa kimataifa – yaani UM na wawakilishi wa Afrika – kuhusu taratibu za kuwapatia raia wa Darfur hifadhi ziada na kukomesha vitendo vya uhalifu dhidi yao na kuhakikisha maamuzi na madaraka ya Mahakama juu ya suala hilo yanatekelezwa haraka kwenye eneo la mtafaruku la Sudan magharibi.

Hapa na pale (Taarifa za Kusoma)

Mohamed ElBaradei, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Kimataifa juu ya Matumizi ya Amani ya Nishati ya Nyuklia (IAEA) Ijumatatu aliwaambia wajumbe wa Bodi la Magavana wa taasisi waliokutana Vienna, kwamba wakaguzi wake wameweza kuthibitisha Iran haijabadilisha matumizi ya nyuklia kinyume na dhamira ilioripotiwa nao. Kadhalika ElBaradei alisema IAEA haikufanikiwa kuthibitisha madai ya baadhi ya mataifa kwamba mradi wa nishati ya nyuklia wa Iran, unafungamana na shughuli za kijeshi. Aliyataka yale Mataifa Wanachama yenye kudai kuwa na ushahidi mradi wa Iran wa nyuklia hutumiwa kwenye shughuhuli za siri za kijeshi yaipatie IAEA ushahidi huo ili uthibitishwe na wataalamu wake kama ni ushahidi wa kweli au la.

UM unaadhimisha Siku ya Amani Kimataifa

Umoja wa Mataifa unaadhimisha Siku ya Amani Kimataifa kwa kuandaa tafrija kadha wa kadha zilienedelezwa katika Makao Makuu mjini New York, na kwenye maeneo mengine ya dunia. KM Ban Ki-moon alijumuika na watu mashuhuri kadha walioteuliwa kama Wajumbe wa Amani wa UM, pamoja na Raisi wa Baraza Kuu na watumishi wa UM kwenye tafrija maalumu ya kila mwaka ambapo KM aligonga kengere ya amani iliopo kwenye bustani ya UM.

'Vifo vya uzazi katika nchi maskini ni msiba usiostahamilika' imehadharisha UNICEF

Shirika la UM juu ya Mfuko wa Maendeleo kwa Watoto (UNICEF) umetoa ripoti juu ya vifo vya uzazi ambavyo hukutikana zaidi miongoni mwa mama waja wazito katika mataifa yanayoendelea. Ripoti iliopewa mada isemayo “Maendeleo ya Watoto: Fafanuzi juu ya Udhibiti wa Vifo vya Uzazi” ilibainisha kwamba asilimia 99 ya vifo vya uzazi hutukia zaidi katika nchi zinazoendelea, na kati ya idadi hiyo asilimia 84 humakinikia kwenye zile nchi ziliopo kusini ya Sahara na Asia ya Kusini. Mkuu wa Afya wa UNICEF, Dktr Peter Salama aliwaambia waandishi habari Geneva umuhimu wa ripoti.

WHO inasema sigara ya elektroni si tiba ya kukomesha uvutaji sigara

Shirika la Afya Duniani (WHO) limetoa tangazo maalumu lenye kutahadharisha juu ya hatari ya kutumia ile sigara ya elektroni, ambayo watangazaji wa biashara wanadai humpatia mvutaji tiba ya kuwacha kuvuta sigara za kawaida. Kwa mujibu wa WHO madai haya hayana msingi na hayajathibitishwa kisayansi,na kuwataka wachuuzi wa sigara za elektroni waache kudai WHO imeidhinisha matumizi ya sigara hizo.