Kikao cha 63 cha Baraza Kuu la UM chafunguliwa rasmi
Majadiliano ya jumla ya Baraza Kuu la UM, kwenye kikao cha wawakilishi wote yalianzishwa rasmi asubuhi ya leo ambapo viongozi wa kimataifa waliwasilisha hoja zao kadha wa kadha kuhusu utaratibu unaofaa kuzingatiwa kimataifa ili kukabiliana na matatizo ya ulimwengu kipamoja.