WFP inaomba msaada wa kuhudumia chakula mamilioni Ethiopia
Shirika la UM juu ya Miradi ya Chakula Duniani (WFP) limetangaza ilani maalumu ya maombi ya kufadhiliwa dola milioni 460 kuhudumia chakula watu milioni 9.6 katika Ethiopia ambao wameathirika vibaya sana kutokana na ukame uliotanda kwenye maeneo yao ikichanganyika na mifumko hatari ya bei za chakula.